Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga
(Kulia), akisalimiana na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Zanzibar, Ali Malimussy (kushoto), baada ya kuwasili Makao Makuu ya
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Dodoma.
Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar Ali Malimussy,
akisaini kitabu cha wageni wakati walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji jijini Dodoma, akiwa ameambatana na Wakuu wa Vikosi
vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), lengo ni kukuza mahusiano na
ushirikiano kati ya vyombo hivyo, (Kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi
la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga.
Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar Ali Malimussy,
akifafanua jambo, wakati walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji jijini Dodoma akiwa ameambatana na Wakuu wa Vikosi vya
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) mapema leo.
Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Ali Ali (kulia), akimshukuru
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga kwa
niaba ya Ujumbe uliotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo yaliyopo jijini
Dodoma mapema leo.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga (katikati)
akiwa kwenye picha ya pamoja na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na
Uokozi Zanzibar, Ali Malimussy (Wanne kutoka kushoto), Kamishna wa Chuo
cha Mafunzo Zanzibar Ali Ali (Watatu kutoka kushoto), Mkuu wa Kikosi cha
Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Ali hamad ( Wasita kutoka kulia), Wajumbe
toka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Viongozi Waandamizi wa
Jeshi hilo wakati walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji jijini Dodoma mapema leo. (PICHA NA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI)
**********************************
Wakuu wa Vikosi vya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar (SMZ), wakiongozwa na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto
na Uokozi Zanzibar, Ali Malimussy watembelea Makao Makuu ya Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji nchini yaliyopo jijini Dodoma. Lengo ni kukuza
mahusiano na ushirikiano kati ya vyombo hivyo.
Katika ziara hiyo Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga, alitumia
fursa hiyo kuwapongeza Wakuu wa Vikosi hivyo kwa kazi nzuri
wanazozifanya na kuwaahidi ushirikiano katika kulijenga Taifa.
Aidha Kamishna Malimussy
amemshukuru CGF John Masunga kwa niaba ya Ujumbe uliotembelea Makao
Makuu ya Jeshi hilo. “Tumejifunza mengi lakini pia tunashukuru kwa
kupata fursa ya kutembelea na kuona jinsi gani tunaweza kushirikiana”
alisema Kamishna Malimussy.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...