Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.
Jenista Mhagama akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mpango wa Uendelezji
wa Viwanda Vidogo na vya Kati.Uzinduzi ulifanyika jijini Dodoma. Kulia
kwake ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Prof. Joyce Ndalichako,
kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa, na wa
kwanza kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi yake anayeshughulikia Sera, Uratibu
na Uwekezaji Bi. Dorothy Mwaluko anayemfuata ni Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe na wa kwanza kushoto ni Katibu
Mktendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Beng’I
Issa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.
Jenista Mhagama akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa
Uendelezji wa Viwanda Vidogo na vya Kati.Uzinduzi ulifanyika jijini
Dodoma.
Waziri Viwanda na Biashara Mhe.
Innocent Bashungwa akizungumza masuala yanayohusu viwanda na biashara
wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Uendelezji wa Viwanda Vidogo na vya Kati
ulifanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Elimu, Sayansi na
Teknoloji Profesa Joyce Ndalichako,akieleza fursa katika sekta ya elimu
kwa washiriki wa uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii (NSSF),Bw.William Erio akielezea jinsi walivyosaidia
wajasiliamali wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Uendelezji wa Viwanda
Vidogo na vya Kati.Uzinduzi ulifanyika jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Shirika la kuhudumia
viwanda vidogo SIDO Prof.Silvester Mpanduji uzinduzi wa Mpango wa
Uendelezji wa Viwanda Vidogo na vya Kati.Uzinduzi ulifanyika jijini
Dodoma.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Beng’I Issa,akizungumza wakati
wa uzinduzi wa Mpango wa Uendelezji wa Viwanda Vidogo na vya
Kati.Uzinduzi ulifanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe walioshiriki
katika hafla ya Uzinduzi wa Mpango wa Uendelezji wa Viwanda Vidogo na
vya Kati uliofanyika Julai 10, 2020 Ukumbi wa Hazina Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.
Jenista Mhagama, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Profesa Joyce
Ndalichako pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Innocent
Bashungwa wakicheza na kufurahia wimbo maalum wa kuipingeza Serikali
katika mapinduzi ya viwanda ulioimbwa na Msaanii Bw. Mrisho Mpoto wakati
wa hafla hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.
Jenista Mhagama pamoja Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Profesa
Joyce Ndalichako (kuli kwake) na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe
Innocent Bashungwa (kushoto kwake) pamoja na viongozi walioshiriki
katika uzinduzi wa Mpango wa Uedeshaji wa Viwanda Vidogo na vya
KatiJijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.
Jenista Mhagama, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Profesa Joyce
Ndalichako pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Innocent
Bashungwa wakimsikiliza Mama Kaminyoge akitoa maelezo kuhusu vyakula vya
kusindikwa vya aina mbalimbali wakati wa maonesho ya wajasiriamali
walioshiriki katika uzinduzi huo Jijini Dodoma
…………………………………………………………………………………
Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu,
Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama
amezindua Mpango wa Uendelezaji wa Viwanda Vidogo na vya Kati wenye
lengo la kutatua changamoto ya upatikanaji wa ujuzi, masoko na mitaji
katika miradi midogo na vya kati (SMEs) nchini.
Uzinduzi huo
ulifanyika mapema Julai 10, 2020 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage
Hazina Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Waziri wa Viwanda na Biashara
Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa
Joyce Ndalichako, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na
Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na
Biashara Prof. Riziki Shemdoe.
Pia ulihudhuriwa
na baadhi ya Wakuu wa Taasisi za SIDO, VETA, NEEC, NSSF na Banki ya
AZANIA pamoja na Viongozi na Wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali za
Sekta binafsi, Wajasiriamali na Wanafunzi kutoka Vyuo mbalimbali nchini.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Waziri Mhagama amesema uwepo wa mpango huo utasaidia
kuongeza kasi ya ujenzi na ukuaji wa uchumi kwa kutengeneza mazingira
wezeshi na kuandaa mazingira yenye mfumo wa kibiashara yatakayorahisisha
kutengeneza uzalishaji wenye tija na kuunda soko la bidhaa
utakaoboresha na kuinua maisha ya Watanzania.
“Serikali
imetengeneza fursa za kuwezesha wananchi kushiriki katika shughuli
mbalimbali za maendeleo na kujipatia kipato na kuhakikisha
inatatua changamoto mbalimbali zinazokabili nguvu kazi ya taifa ikiwa ni
pamoja na ukosefu wa elimu na ujuzi wa kutosha pamoja na ukosefu wa
mitaji na masoko ya uhakika wa bidhaa zinazozalishwa”,alisema Waziri
Mhagama.
Waziri alifafanua
kuwa mpango umejikita katika kuhakikisha kuwa wajasiriamali wanasaidiwa
kuongeza ujuzi, kupata uzoefu na kuwawezesha kuhimili ushindani katika
masoko ya ndani na nje. Aidha, Mpango huu pia unalenga kuwezesha viwanda
kupata vifaa vya kisasa kama mitambo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji
ili uwe na tija, kutoa mikopo yenye riba nafuu ili kupanua shughuli za
uzalishaji pamoja na kuongeza kinga za hifadhi za jamii kwa
wajasiriamali.
“Kupitia mpango
huu wenye viwanda na wajasiriamali wamepanuliwa fursa ya kupata mitaji
hivyo kutengeneza fursa za ajira kwa vijana wengi wanaohitimu vyuo
katika ngazi mbalimbali,”Alisistiza Waziri
Aliongezea kuwa,
Mfumo unajikita kuwafika wananchi wote bila ubaguzi na matabaka ya aina
yoyote kwa kuzingatia vigezo na masharti nafuu yaliyopo katika mfumo
huu.
“Programu hii
inavunja matabaka baina ya makundi mbalimbali katika jamii na kutoa
fursa sawa kuanzia mtu binafsi hadi vikundi katika kuwapatia mitaji na
ujuzi sawa hivyo tuiunge mkono kwani inawalenga Watanzania wote,”
alisema
Aidha alibainisha
sekta ya viwanda imeendelea kuwa na tija katika kuchangia ongezeko la
Pato la Taifa kwa kuongezeka kwa viwanda vidogo, vya kati na vikubwa
ambapo Sekta ya Viwanda katika Pato la Taifa kwa mwaka 2019 ilikuwa
asilimia 8.5 ikilinganishwa na asilimia 8.05 mwaka 2018, sawa na
ongezeko la asilimia 0.45 na hii ni matokeo ya kuongezeka kwa shughuli
za uzalishaji viwandani katika kipindi hicho pamoja na kasi ya ukuaji wa
thamani ya Uzalishaji Bidhaa Viwandani kwa mwaka 2019 ambayo ilikuwa ni
Shilingi Trilioni 10.2 ikilinganishwa na Shilingi Trilioni 9.6 mwaka
2018, sawa na kasi ya ukuaji wa asilimia 5.8
Waziri aliendelea
kutoa wito kwa taasisi husika kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu
fursa zilizopatikana katika program na kuvitumia vyombo vya habari
katika kueleimisha umma kwa malengo ya kuwafikiwa wengi pamoja na
kuzitaka taasisi za kibenki kutoa mikopo kwa wajasiriamali kwa mifumo
rafiki na inayofikika pamoja na kuutaka uongozo wa Baraza la Taifa la
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kuwa na program za tathimin utekelezaji wa
mpango kwa vipindi mbalimbali.
Naye Waziri wa
Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa alieleza furaha yake ya
uwepo wa mpango huo kwani umesadifu mikakakti ya nchi katika uendelezaji
viwanda na kusema imekuja wakati mwafaka kwa kuzingatia imelenga sekta
zenye tija katika kutoa ajira kwa watanzania wengi kwani imefungamanisha
sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuwa ndizo zenye mchango mkubwa
katika ajira.
“Ni hakika kuwa,
kupitia Mpango huu wa uendelezaji wa viwanda, ajira za moja kwa moja na
zisizo za moja kwa moja katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta za
kilimo, uvuvi na ufugaji zitaongezeka na kupunguza changamoto mbalimbali
zinazokabili jamii kutokana na ongezeko la wasio na ajira
nchini,”Alisema waziri Bashungwa.
Kwa upande wake
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi,
Beng’I Issa alisema, mpango umeainisha namna bora ya kuwawezesha
wananchi kiuchumi ikiwemo la kukuza mitaji na kuimarisha vyanzo vyao vya
mapato na kukuza akiba na mikopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...