NA DENIS MLOWE,IRINGA

ZAIDI ya wanachama 250 wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika majimbo na kata za uchaguzi wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kwa siku mbili tangu kuanza rasmi utolewaji wa fomu kwa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na wanahabari Katibu wa CCM wilaya ya Mufindi James Mgego alisema kuwa wanachama wengi wamejitokeza tangu kuanza kutolewa fomu za kuomba kuteuliwa siku ya jana kutokana na wengi wao kuwahiwa kuongoza majimbo mbalimbali na kata katika wilaya hiyo.

Alisema kuwa uwingi wa wachukua fomu ndani ya chama hicho ni haki ya kila mwanachama anayetakiwa kuchagua au kuchaguliwa na kuonyesha ni kiasi gani CCM wanademokrasia ya kweli ndani ya chama na wito wa huo imeonyesha kuwa chama hicho kina viongozi wengi imara ambao wakichaguliwa watawaletea maendeleo wananchi.

Mgego alisema kuwa wanachama wengi wamechukua fomu kwenye ngazi ya kata ambao wanaomba kuteuliwa kuwa madiwani ambapo hadi kufikia leo majira ya saa nne asubuhi wamekwisha jitokeza wanachama 119 ambapo wataongezeka pindi mwisho wa kurudisha fomu za kura za maoni utakapokwisha.

Alisema kuwa kufikia leo wagombea wa nafasi za ubunge katika majimbo ya Mufindi wamefikia idadi ya wachukua fomu 80 ambapo jimbo la Mufindi Kusini limeonekana kuwa kinara kwa wagombea zaidi ya 24 kujitokeza ambapo siku ya kwanza ya uchukuaji fomu walikuwa wachukua fomu 17 hali ambayo itaendelea kwa wagombea kujitokeza zaidi.

Aliongeza kuwa jimbo la Mufindi Kaskazini wagombea wamejitokeza kwa wingi ambapo idadi yao imefikia 17 na wanaendelea kujitokeza kuchukua fomu jimbo ambalo lilikuwa chini ya mbunge Mahamud Mgimwa.

Kwa upande wa jimbo la Mafinga mjini wagombea waliojitokeza kumpima alyekuwa mbunge wa jimbo hilo Cosato Chumi ni wagombea 9 ambapo wengi wao walichukua fomu siku ya kwanza na wanatarajia kuongezeka hadi kufikia idadi ya watia nia 15 hadi mwisho wa kurudisha fomu.

Mgego aliwataadharisha wagombea wote ambao wanamlengo wa kutoa rushwa kwa wajumbe kuacha mara moja kwani chama kiko imara na mgombea yoyote atakayebainika kufanya rafu kwenye kura za maoni chama hakitasita kulikata jina lake na kuwataka kufanya yaliyondani ya kanuni na katiba za chama.

Baadhi ya waliochukua fomu na kutaka kuteuliwa na mwanahabari hizi kuwashuhudia ni, Ayoub Sanga, Marco Ng’umbi (Mkalimoto),Modestus Kisoso John Malata na kwa upande wa udiwani wa viti maalum Grace Mgina amechukua fomu za kutaka kuteuliwa. 
James Mgego Katibu wa CCM wilaya ya Mufindi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...