Mganga Mkuu wa Jeshi la Magereza, SACP. Hassan Mkwiche akiwasili leo Agosti 11, 2020 katika Gereza la Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro akiwa ameongozana na msafara wa Timu ya wataalam(hawapo pichani)kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya. Kushoto kwake ni Mkuu wa Gereza Rombo, ASP. Lucas Mboje.

 Mkuu wa Gereza Rombo, ASP. Lucas Mboje akiwa ameongozana na Timu ya wataalam kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya ambao leo wameendesha Mafunzo ya kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu magerezani kwa maofisa na askari wa Gereza Rombo.
 . Mganga Mkuu wa Jeshi la Magereza, SACP. Hassan Mkwiche(katikati) akitoa maelezo mafupi kabla ya kuwakaribisha wataalam kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya kutoa mafunzo ya kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu magerezani kwa maofisa na askari wa Gereza Rombo. Kulia ni Naibu Mkurugenzi kutoka  Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya(kushoto) ni Dkt. Wilbard Mhandiki.
 Mtaalam kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Emmanuel Matechi akitoa historia ya ugonjwa wa kifua kikuu kwa washiriki.
 Maafisa na askari wa Gereza Rombo wakifuatilia mafunzo ya kudhibiti kifua kikuu magerezani.
Timu ya wataalam kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya wakifuatilia mafunzo hayo.
  Washiriki wa mafunzo ya kudhibiti kifua kikuu magerezani kutoka Gereza Rombo wakiwa katika picha ya pamoja na wataalam  kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu - Wizara ya Afya leo mara baada ya mafunzo leo Agosti 11, 2020(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...