Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joseph Mkirikiti akizungumza na viongozi wa
chama cha wachimbaji madini wa mkoa huo (MAREMA) walipotembelea ofisini
kwake kujitambulisha kwenye ziara yao ya kutembelea machimbo na kutatua
changamoto mbalimbali za wachimbaji madini, kulia ni Mwenyekiti wa
MAREMA Justin Nyari na Katibu wa MAREMA Tariq James.
Mwenyekiti
wa chama cha wachimbaji madini wa Mkoa wa Manyara, (MAREMA) Justin
Nyari (wapili kulia) akizungumza na Ofisa madini mkazi wa mkoa huo
Godfrey Nyanda, baada ya viongozi wa Marema kutembelea ofisini kwake
kwenye ziara yao ya kutembelea machimbo na kutatua changamoto mbalimbali
za wachimbaji madini, kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa MAREMA, Money
Yusuf na kulia ni Katibu Msaidizi wa MAREMA, Joseph Manga.
******************************
Na Mwandishi wetu, Babati
VIONGOZI wa chama
cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) wameanza ziara ya wiki
mbili kutembelea wachimbaji mbalimbali wa madini kwenye Wilaya za
Babati, Mbulu, Kiteto, Hanang’ na Simanjiro.
Mwenyekiti wa
MAREMA Justin Nyari akizungumza jana mjini Babati alisema lengo la ziara
hiyo ni kutembelea machimbo mbalimbali kwa lengo la kukagua usalama
migodini, afya na mazingira.
Nyari alisema pia
wataangalia suala zima la tozo na kodi za serikali, matumizi ya baruti,
uhai wa leseni, mikataba na vitambulisho wachimbaji wasio rasmi na
wanachama wapya.
Makamu Mwenyekiti
wa MAREMA, Money Yusuf alisema watakutana na wanachama mbalimbali wa
chama hicho wa eneo hilo kwa lengo la kutambua changamoto zao na
kuzitatua zile zilizopo ndani ya uwezo wao.
“Wanachama wetu
huwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo tunawafuata kwenye
matawi yao kwa ajili ya kuwasikiliza na kuzungumza nao,” alisema Yusuf.
Katibu wa MAREMA,
Tariq James alisema pia watafika kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo
Joseph Joseph Mkirikiti kwa ajili ya kufahamiana naye ili kushirikiana
katika kuhudumia wachimbaji.
James alisema pia watakutana na ofisa madini mkazi wa mkoa huo Godfrey Nyanda ambaye ndiye mlezi wa MAREMA katika eneo hilo.
Mweka hazina wa
MAREMA, Neney Lyimo alisema katika ziara yao watatembelea maeneo
mbalimbali ikiwemo ile yenye migogoro ya wachimbaji na hifadhi za
Taifa.
“Tutafuatilia
migogoro ya wachimbaji wa madini ya Green Aventurine wa kijiji cha
Sangaiwe na hifadhi ya Taifa ya Tarangire na wachimbaji wa madini ya
Alexander light wa kijiji cha Mayoka na hifadhi ya Ziwa Manyara,”
alisema.
Katibu msaidizi
wa MAREMA, Joseph Manga alisema wao kama viongozi wameonelea wasikae
ofisini pekee ila wawafuate wanachama kwenye matawi yao mbalimbali.
“Tukiwa viongozi
wa MAREMA ni muhimu kuwafikia wanachama wetu na kusikiliza kero,
changamoto na ushauri wao kwenye sekta hii ya madini,” alisema Manga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...