Naibu Waziri wa Ardhi
Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemtembelea Mjane wa Baba wa
Taifa Julius Kambarage Nyerere Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Butiama mkoa
wa Mara.
Dkt Mabula alikuwa katika
ziara ya siku moja wilayani Butiama kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi
sambamba na kugawa hati za ardhi kwa wananchi wa Butiama mkoani Mara waliopimiwa
na kumilikishwa maeneo yao.
Naibu Waziri mbali na
kutembelea wilaya ya Butiama pia alitembelea wilaya za Musoma, Rorya na Tarime ambako
alizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi, alikagua mfumo wa ukusanyaji kodi
ya pango la ardhi na kufuatilia maelekezo aliyoyatoa kuhusiana na masuala ya
ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula
akimsikiliza mjane wa Baba wa Taifa Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere Bi
Maria Nyerere alipomtembelea nyumbani kwake Butiama mkoa wa Mara jana wakati akiwa
katika ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiagana
na mjane wa Baba wa Taifa Hayati Mwl
Julius Kambarage Nyerere Bi Maria Nyerere alipomtembelea nyumbani kwake Butiama
mkoa wa Mara jana wakati akiwa katika ziara
yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Dkt Angeline Mabula akimkabidhi Hati ya Ardhi Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha
Mwl Nyerere Profesa Agnes Mwakaje alipokuwa katika ziara yake ya kukagua
utendaji kazi wa sekta ya ardhi mkoa wa Mara jana.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa
katika picha ya pamoja na wananchi wa Butiama mkoa wa Mara baada ya kuwakabidhi
Hati ya Ardhi jana wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta
ya ardhi mkoa wa Mara (PICHA ZOTE NA
WIZARA YA ARDHI).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...