Na Amiri Kilagalila,Njombe
Waandishi wa habari mkoani Njombe wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga dhidi ya virusi vya corona (Covid-19) vinavyosababisha homa kali ya mapafu,pindi wanapo kuwa katika majukumu yao ya kazi pamoja na kuendelea kuhabarisha umma kuendelea kuchukua tahadhari hiyo.
Licha Taifa la Tanzania kuwa salama dhidi ya virusi vya Corona kutokana na kuondolewa hofu ya virusi hivyo,wito umetolewa na Bi,Eveline Kidenya afisa afya wilaya ya Njombe kwa makundi mbalimbali likiwemo kundi la waandishi wa habari kuendelea kuchukua tahadhari hasa pindi wanapokuwa katika mikusanyiko.
“Tuwe huru,tuishi na kirusi hicho kama tunavyoishi na virusi wengine au Bakteria wengine,cha msingi tusipuuzie kuendelea kuchukua tahadhari tunapokutana na wageni ambao sio wana Njombe kwa kuwa kama Njombe tuko salama tusifikiri na watu wa maeneo mengine wako salama”alisema Bi Eveline Kidenya
Umoja wa vyama vya waandishi wa habari Tanzania kwaufadhili wa nchi ya sweedeni kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe NPC wametoa mafunzo hayo dhidi ya kujikinga na Corona kwa waandishi wa habari wanachama kupitia wataalamu wa afya ofisi ya mganga mkuu wa wilaya ya Njombe.
“Tumepata mafunzo haya ambayo yapo katika mpango mkakati wa UTPC umoja wa vyama vya waandishi wa habari Tanzania wakipata ufadhili kutoka ubalozi wa Sweeden kwa ajili ya kutuwezesha waandishi wa habari kutoa habari lakini vile vile kujikinga na maambukizi haya ya Corona”alisema Hamis Kassapa katibu wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe NPC
Erasto Mgeni na Emiria Msafiri ni baahi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika semina hiyo wamesema wamepokea vema mafunzo hayo huku wakiadhi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi namna ya kundelea kuchukua tahadhari ili kujikinga na virusi hivyo.
Waandishi wa habari mkoani Njombe wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga dhidi ya virusi vya corona (Covid-19) vinavyosababisha homa kali ya mapafu,pindi wanapo kuwa katika majukumu yao ya kazi pamoja na kuendelea kuhabarisha umma kuendelea kuchukua tahadhari hiyo.
Licha Taifa la Tanzania kuwa salama dhidi ya virusi vya Corona kutokana na kuondolewa hofu ya virusi hivyo,wito umetolewa na Bi,Eveline Kidenya afisa afya wilaya ya Njombe kwa makundi mbalimbali likiwemo kundi la waandishi wa habari kuendelea kuchukua tahadhari hasa pindi wanapokuwa katika mikusanyiko.
“Tuwe huru,tuishi na kirusi hicho kama tunavyoishi na virusi wengine au Bakteria wengine,cha msingi tusipuuzie kuendelea kuchukua tahadhari tunapokutana na wageni ambao sio wana Njombe kwa kuwa kama Njombe tuko salama tusifikiri na watu wa maeneo mengine wako salama”alisema Bi Eveline Kidenya
Umoja wa vyama vya waandishi wa habari Tanzania kwaufadhili wa nchi ya sweedeni kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe NPC wametoa mafunzo hayo dhidi ya kujikinga na Corona kwa waandishi wa habari wanachama kupitia wataalamu wa afya ofisi ya mganga mkuu wa wilaya ya Njombe.
“Tumepata mafunzo haya ambayo yapo katika mpango mkakati wa UTPC umoja wa vyama vya waandishi wa habari Tanzania wakipata ufadhili kutoka ubalozi wa Sweeden kwa ajili ya kutuwezesha waandishi wa habari kutoa habari lakini vile vile kujikinga na maambukizi haya ya Corona”alisema Hamis Kassapa katibu wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe NPC
Erasto Mgeni na Emiria Msafiri ni baahi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika semina hiyo wamesema wamepokea vema mafunzo hayo huku wakiadhi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi namna ya kundelea kuchukua tahadhari ili kujikinga na virusi hivyo.
Baadhi ya waandishi wa
habari wa mkoa wa Njombe,wawakilishi kutoka vyombo mbambali vya habari nchini
Tanzania wakati wakikumbushwa mambo mbali mbali juu ya magonjwa ya mlipuko
hususani mambukizi ya virusi vya Corona katika semina iliyofanyika hii leo
ukumbi wa Dosmeza mjini Njombe.
Bi,Eveline Kidenya
afisa afya wilaya ya Njombe wakati akitoa maelekezo juu ya magonjwa ya mlipuko
na virusi vya Corona.
Katibu wa Chama cha
waandishi wa habari mkoa wa Njombe NPC Ndugu Hamis Hassan Kasapa akizungumza
jambo mbele ya waandishi wa habari wakati wa semina ya siku moja juu ya
kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya milipuko hususani Corona.
Waandishi wa habari
mkoa wa Njombe wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya semina ya
kuelimishana namna ya kujikinga dhidi ya magonjwa ya milipuko hususani ugonjwa
wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...