Mgombea Ubunge jimbo la Mkuranga, Abdallah Hamisi Ulega (kushoto) akizungumza na wanachama wa Chama cha Mapindunzi na Wananchi wa Tarafa  ya Mkamba.(Picha na Emmanuel Massaka michuzi Tv)

Wananchi wakimsikiliza mgomea ubunge jimbo la Mkuranga.
Mwanachama mpya wakipokea Kadi za CCM


WANANCHI wa tarafa ya Mkamba wilayani Mkuranga mkoani Mkuranga Pwani wameahidiwa kupatiwa gari ya kubebea wagonjwa katika kituo cha afya mkamba kilicho boreshwa ikiwa ni pamoja na kujaziwa vifaa, na kuletewa daktari wa upasuaji ili kuendelea kutoa huduma bora. 

Aahadi hiyo imetolewa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mkuranga na Naibu Waziri wa Mifugo Na Uvuvi,Abdallah Ulega wakati alipofanya kampeni katika Kata ya Mkamba, Pupu na Panzuo zilizopo katika tarafa ya mkamba na kusema kituo cha afya Mkamba kilikuwa na halimbaya wakati anaingia madarakani lakini kwa juhudi za Daktari John Pombe Magufuli Sasa kimeboreshwa. 

Ulega amesema ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi kupitia ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 21/25 kila kituo cha afya nchini kitapatiwa gari kwa ajili ya kubebea wagonjwa. 

Kwa upande mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mkuranga,Ally Msikamo aliposimama kuwaombea kura wagombea wachama cha mapinduzi akiwemo Rais, mbunge na diwani amesema 

Hata hivyo Ulega amesema anaenda kuinua kiwango cha elimu mkamba kwa kujenga Shule ambapo ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Nyekenge, lengo nikuhakikisha Mkamba inapata wasomi wengi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...