Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Bw. Rashidi Kassim alipowasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya kujitambulisha, kabla hajaanza ziara ya kukagua miradi ya miundombinu inayoratibiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna wa Polisi Thobias Andeng'enye akiwa katika kikao cha kupeana taarifa kuhusu mkoa huo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Kanali Michael Ngayalina kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi, Eneo la Manyovu ambapo kutajengwa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP). |
|
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akimsikiliza Mshauri Mwelekezi wa ujenzi wa mradi wa Barabara kutoka Kasulu hadi Kibondo ambao unajengwa na Mkandarasi kutoka China kwa fedha za mkopo nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika. |
Bi. Edna Chuku akibadilishana mawzo na Mhandisi wa TANROADS wa Mkoa wa Kigoma walipokuwa kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma. |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...