Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Joseph Mapunda(katikati) akisoma hukumu ya Radio Ihsaan FM ya kukiuka maudhui ya utangazaji ambapo radio hiyo imepigwa sh.milioni Tano jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeipiga faini ya sh.milioni Tano Ihsaan Redio FM kutokana na kukiuka maudhui ya utangazaji.
Kituo hicho cha Redio kinatakiwa kuomba radhi kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 28 na kipindi cha Al Jawaabul kikifika hawatakiwi kurusha matangazo ya aina yeyote zaidi ya kuomba radhi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Joseph Mapunda amesema Kituo hicho cha Redio kinatakiwa kuwa na waandishi wenye taaluma hiyo pamoja na kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wao.
Mapunda amesema kuwa wasiporidhika na hukumu hiyo wanaweza kukata rufaa katika Tume ya Ushindani (FCC).
Aidha amesema Kituo hicho kinatakiwa kufuata Sheria za maudhui ya Utangazaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...