Viongozi Wa Dini Wa Kamati ya Amani wamelaani vikali vitendo vya baadhi ya Viongozi Wa Dini kutumia Madhabahu na Nyumba za ibada kufanya kampeni za kuwanadi viongozi Wa Dini jambo ambalo ni kinyume na maadili.


Akizungumza na waandishi Wa habari leo, Mwenyekiti Wa kamati hiyo ambae pia ni Sheikh Wa Mkoa Wa Dar es salaam Alhad Mussa Salum amesema kama vitendo hivyo vitafumbiwa macho vinaweza kuhatarisha hali ya amani na kuwagawanya waumini wanaokwenda kusali.


Aidha amesema Kama kiongozi Wa dini anaona mgombea fulani anamfaa ni vyema akaenda kwenye majukwaa ya siasa ili kumnadi lakini sio kutumia nyumba za ibada kunadi wanasiasa.


Katika mkutano huo pia umehudhuriwa na Wajumbe Wa kamati ya amani ikiwemo Maaskofu, manabii, wachungaji, Maimamu na Mashaikh ambapo wote kwa pamoja wamaonyesha Kutokufurahishwa na vitendo hovyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...