Na. Lusajo Frank, DSJ
WAZIRI wa Afya wa Uingereza, Matt Hancock amesema maambukizi ya virusi vya Corona yanaongezeka nchini humo huku uandikishaji wa wagonjwa wapya ukiongezeka maradufu kila siku.
Uingereza imeripoti idadi kubwa ya vifo vilivyotokana na COVID-19 ulimwenguni, baada ya Marekani, Brazil, India na Mexico, kulingana na data iliyokusanywa na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins.
"Idadi ya watu hospitalini inaongezeka maradufu kila baada ya siku nane au zaidi, tutafanya kile kinachohitajika ili kuwaweka watu salama." alimekuliwa Hancock
Waziri Mkuu Boris Johnson alikosolewa na wanasiasa wa upinzani kwa kushindwa kudhibiti mlipuko wa Corona hata hivyo serikali imejitahidi kuhakikisha upimaji wa kutosha katika wiki za hivi karibuni.
Kesi za COVID-19 zilianza kuongezeka tena nchini Uingereza mnamo Septemba, na kati ya visa 3,000 na 4,000 vyema vilirekodiwa kila siku katika wiki iliyopita, siku ya Alhamisi, Uingereza ilirekodi vifo 21 vilivyotokana na ugonjwa wa Corona.
Uingereza hivi karibuni ilipitisha sheria ya kuzuia mikusanyiko. Lakini wakosoaji wamesema hatua hii haikutosha, kudhibiti maambukizi ya Corona.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...