Charles James, Michuzi TV

VIONGOZI mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole na Mgombea Ubunge Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile wamejitokeza katika kituo cha kupiga kura cha Kilimani jijini Dodoma kupiga kura ya kuchagua Rais, Mbunge na Diwani huku wakieleza kuridhishwa na muamko wa wananchi pamoja na hali ya amani na utulivu iliyopo.

Akizungumza baada ya kupiga kura Dk Bashiru amewataka watanzania kuzidi kujitokeza kwa wingi kwenye vituo walivyojiandikisha ili waweze kutimiza haki yao ya Msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Kwa upande wake Polepole ameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuwapokea wananchi na kuelekeza ili waweze kupiga kura bila usumbufu wowote.

" Nimeridhika na hali ya utulivu, wananchi wamehamasika sana na uchaguzi huu, niwaombe wanaokuja vituoni kupiga kura wakishamaliza warudi majumbani mwao wasubiri matokeo," Amesema Ditopile.

Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally akiwa kwenye foleni ya kupiga kura katika kituo cha Kilimani jijini Dodoma. Wa mwisho ni Mgombea Ubunge Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile.


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole (wa kwanza kulia) akiwa na Mgombea Ubunge Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile (katikati) wakipata maelekezo kutoka kwa msimamizi wa kituo cha kupiga kura cha Kilimani jijini Dodoma.

Wananchi mbalimbali wakiwa kwenye foleni ya kupiga kura katika kituo cha kupiga kura cha Kilimani jijini Dodoma leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...