Na Said Mwishehe,Michuzi TV- Arusha

WAZIRI Mkuu mstaafu Edward Lowassa pamoja na Katibu Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Abdulrahman Kinana wamemuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya Chama hicho Dk.John Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Arusha Mjini.

Wakizungumza mbele ya maelfu ya wananchi wa Jiji la Arusha  wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea urais Dk.Magufuli ambaye leo amewaomba kura wananchi wa Mkoa wa Arusha ili achaguliwe tena kuongoza nchi kwa miaka mingine mitano.

Kinana na Lowassa walipata nafasi ya kuzungumza na kumuombea kura baada ya Dk.Magufuli kuwaomba viongozi hao wastaafu kuwasalimia wananchi waliokuwepo katika mkutano huo.

Kinana alikuwa wa kwanza kuzungumza na kisha kumuombea kura Dk.Magufuli ambapo anesema anaunga na Wana CCM wengine kumuombea kura mgombea huyo ambaye kwa kipindi cha miaka mitano amefanya mambo makubwa ya maendeleo.

Amefafanua Dk.Magufuli ameweza kutekeleza ahadi zote ambazo ziliahidiwa na CCM katika uchaguzi mkuu mwaka 2015, ametekeleza ahadi zote alizoahidi akiwa katika ziara zake za mikoani, na sasa anatoa ahadi nyingine kupitia Ilani ya CCM yenye kurasa 303,hivyo kuna kila sababu ya kumchagua Oktoba 28 mwaka huu.

Kwa upande wake Lowassa hivi sasa kuna nchi kadhaa ikiwemo ya Venazuela na Nigeria kuna vurugu kwa mambo ambayo yanaleta amani nchini Tanzania."Kupitia kwa Mwenyezi Mungu,Rais wetu amepewa jukumu la kuangalia mambo katika nchi hii amekuja na ndoto sahihi kwamba madhara hayo hayaji kwetu...amejitahidi na wananchi wameelewa,"amefafanua Lowassa.

Amesema kwa mambo makubwa ambayo yamefanywa na Rais,zawadi pekee ambayo wananchi wanatakiwa kumpa ni kumpigia kura Oktoba 28 ambayo ndio siku ya Uchaguzi Mkuu nchini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...