Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mgombea Urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi alipowasili katika
mkutano wa kampeni za uchaguzi Mkuu uliofanyika leo katika Uwanja wa
Dole Wilaya ya Magharibi”A”{Picha na Ikulu} 22/10/2020.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) alipokuwa akihutubia na
kumnadi Mgombea wa Urais wa Zanzibar,Wabunge.Wawakilishi na Madiwani
katika mkutano
wa kampeni za uchaguzi Mkuu wa Wilaya ya Dimani na Mfenesini Kichama
uliofanyika leo katika Uwanja wa Dole Wilaya ya Magharibi”A”. {Picha na Ikulu} 22/10/2020. Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Dimani na Mfenesini kichama wakiwa katika katika
mkutano wa kampeni za uchaguzi Mkuu uliofanyika leo katika Uwanja wa
Dole Wilaya ya Magharibi”A” ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).{Picha na Ikulu} 22/10/2020.
Wagombea Ubunge na Uwakilishi wa Wilaya
ya Dimani na Mfenesini kichama wakienda kutunza wakati wa utenzi
uliosomwa na KIJANA wa CCM Hajra Fadhil (hayupo pichani) katika
mkutano wa kampeni za uchaguzi Mkuu uliofanyika leo katika Uwanja wa
Dole Wilaya ya Magharibi”A” ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.{Picha na Ikulu} 22/10/2020.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akiwanadi
Wagombea wa Ubunge.Uwakilishi na Madiwani katika mkutano
wa kampeni za uchaguzi Mkuu wa Wilaya ya Dimani na Mfenesini Kichama
uliofanyika leo katika Uwanja wa Dole Wilaya ya Magharibi”A”. {Picha na Ikulu} 22/10/2020. Mgombea Urais
wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi alipokuwa
akiwapungia mkono wanaCCM mara alipowasili katika viwanja vya mkutano wa
kampeni za Uchaguzi Mkuu Dole Wilaya ya Magharibi “B” Mkoa wa Mjini
Magharibi uliofanyika leo katika Uwanja wa Dole Wilaya ya
Magharibi”A”,[Picha na Ikulu] 22/10/2020.
****************************************
MGOMBEA Urais wa
Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema endapo atapata
ridhaa ya wananchi na kuwa rais, ataimarisha maslahi ya watumishi wa
umma kwa kuongeza mishahara na posho kwa wakati.
Aliwataka wafanyakazi
hao wa umma kuwa tayari kufanya kazi kwa bidii kwani wataboteshewa
maslahi yao lakini watafanya kazi kwa kasi zaidi.
Ahadi hiyo aliitoa
katika mwendelezo wa kampeni za CCM za kuwanadi wagombea wa CCM na
kufafanua Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025 huko katika kiwanja cha
Dole Unguja.
Alisema mbali na
kuimarisha maslahi ya makundi yote ya kijamii ikiwemo maslahi ya
watumishi wa umma, pia atapitia upya maslahi ya wastaafu ili wapate
pencheni kubwa kuliko wanayopata hivi sasa.
Aliwambia wananchi kuwa atalinda umoja wa kitaifa na kudhibiti vitendo vya ubaguzi wa kidini,kisiasa,kikabila.
“Nitadhibiti vitendo
vya ukabila hapa kwetu kuna Upemba na Uunguja yote hayo nitayaondosha
ili wote tuendelee kuwa wamoja”,alisema Dk.Hussein.
Dk.Hussein,alisema
anaipongeza serikali ya awamu ya saba kwa hatua kubwa iliyopigwa katika
sekta ya elimu kwa kujenga skuli za kisasa zenye vifaa vya masomo ya
sayansi katika Mkoa huo
Alisema licha ya mafanikio hayo bado kuna changamoto za uchache wa madarasa na madawati mambo yanayotafutiwa ufumbuzi.
Alisema pia kuna upungufu wa walimu wa sayansi na masomo mengine chanfamoto itakayotafutiwa ufumbuzi.
Alisema serikali hiyo imejenga vituo vya afya vya kisasa vinavyotoa huduma bora kwa wananchi.
Alisema katika mkoa
huo kuna vyanzo vingi vya maji safi na salama licha ya kuwepo na
changamoto ya ubovu na uchakavu wa baadhi ya miundombinu na zitatafutiwa
ufumbuzi.
Alitumia mkutano huo kujiombea kura na kuwaombea kura wagombea wote wa CCM aliwemo Dkt.John Pombe Magufuli.
Makamu Mwenyekiti wa
CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alisema Zanzibar imekuwa huru toka mwaka
1964 baada ya kufanyika mapinduzi ya mwaka 1964 na kwamba wananchi
wanatakiwa kulinda tunu hiyo kwa kuichagua CCM.
Alisema mapinduzi hayo ni kielelezo tosha cha kulinda muungano na amani ya nchi.
Alisema mapinduzi hayo ndio msingi wa maendeleo ya nchi.
Alieleza kwamba baada ya mapinduzi serikali
iliyoongozwa na rais wa kwanza marehemu Abeid Aman Karume,iliasisi
mikakati ya maendeleo zikiwemo sera za elimu, bure,afya bure na kugawa
ardhi bure kwa wananchi.
Katika maelezo yake Dk.Shein,alikemea vitendo
vya kuwajeruhi wanachama wa CCM vinavyofanyika nchini katika maeneo
mbalimbali na kuviita ni vitendo vya kihuni visivyofaa katika siasa za
vyama vingi.
Alisema vyama vya siasa vishindane kwa sera na sio kuumizana kwani vitendo hivyo vinaweza kusababisha machafuko ya kisiasa.
Alieleza kwamba Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ni ya kiungwana wala haina malengo ya kuwaumiza wananchi badala
yake itaendelea kufuata Katiba ya nchi na sheria ili kuendeleza amani
iliyopo.
Aliwataka wananchi kuwa na amani na wajitokeze
kwa wingi kupiga kura ifikapo octoba 28,mwaka huu kwani ulinzi
umeimarishwa kila sehemu.
Pamoja na hayo Dk.Shein,aliwaombea kura wagombea wa wa Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi za Urais ,Ubunge,Uwakilishi na madiwani.
Naye Naibu Katibu
Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi,amesema CCM inalaani vikali
vitendo vya uvunjifu amani vinavyofanywa na watu wanaosadikiwa kuwa
wapinzani vya kuwajeruhi wanachama wa chama hicho.
Dk.Mabodi, alivitaka
vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki za kuthibiti vitendo
hivyo visiendee na kwamba CCM haitolipiza kisasi bali itaendelea kudai
amani mpaka wanashinda kwa kura nyingi na kuingia ikulu.
Alisema CCM
imefanikiwa kuwafikia wananchi wa makundi mbalimbali katika kampeni zake
kwa lengo la kueleza sera imara na kuwaomba kura ili waichague ifikapo
octoba 28 ,mwaka huu.
Mwenyekiti wa jumuiya
ya Wazazi Taifa ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa Magharib kichama
Dkt.Edmund Mndolwa amesema sababu ya CCM kushinda ni kuwa na ilani
inayotekelezeka ambayo ndio mkataba wa CCM na wananchi muongozo ambao
umetekelezwa kwa ufanisi mkubwa.
Alisema wananchi
wanatakiwa kuichagua CCM ili kuwapa fursa viongozi wa CCM wamalizie
miradi na mambo ambayo walikuwa hawajamaliza katika ilani iliyopita na
yamaliziwe katika ilani mpya.
Alisema wananchi
wanatakiwa kulinda amani ya nchi ili nchi iendelee kupiga hatua kubwa za
kimaendeleo ambapo Tanzania imekuwa ni kisiwa cha amani barani afrika.
Alisema Tanzania ni nchi ya 28 kwa kutumia vizuri fedha za umma kwa maendeleo ya taifa.
Mwenyekiti wa Chama
Cha Mapinduzi Mkoa wa Magharib kichama, Mohamed Rajab Soud alisema
katika uongozi wa serikali ya awamu ya saba chini ya Dk.Ali Mohamed
Shein amejenga vituo vya afya vilivyosaidia kupunguza usumbufu kwa
wananchi kufuata huduma za afya nje ya mkoa huo.
Alisema mkoa huo kwa
sasa unang’ara kwa miundombinu ya barabara za lami kila sehemu hali
inayosaidia kuwarahisishia wananchi kusafiri kwa haraka kutoka sehemu
moja kwenda nyingine.
Alisema ungozi huo pia umejenga shule mbalimbali za ghorofa zenye miundombinu mbalimbali.
Mkutano huo umezishirikisha wilaya mbili ambazo ni Mfenesini na Dimani kichama
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...