Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Edwin Rutageruka amefungua kikao cha Wadau wa Kliniki ya Biashara kutoka Taasisi Binafsi na Taasisi za Umma zikiwemo EPZA, BRELA, TIC, GS1, TRA, WMA, NBC, NEEC, TBS, SIDO, FFC, CBE, na TFS. Lengo la kikao hicho ni kufanya tathimini na kujadili mikakati ya maboresho ya utoaji huduma ya Kliniki ya Biashara.
Kliniki ya Biashara husimamiwa na TanTrade na kudhaminiwa na Benki ya NBC ambapo huwakutanisha wataalamu wa Biashara kutoka Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi ambao hushirikiana katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wafanyabiashara nchi.
Itakumbukwa kuwa tarehe 14 Oktoba, 2020 Tanzania kupitia huduma ya Kliniki ya Biashara inayosimamiwa na TanTrade ilitajwa kuwa mshindi wa tatu wa dunia(Best use of partnership category) na wa pekee kutoka nchi za Afrika kwenye Tuzo za Taasisi zinazosimamia Biashara duniani (WTPO Awards 2020.)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...