Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Same
MRADI
wa maji wa Bwawa la Mungu ambao ulitakiwa kukamilika mwaka 2017 ,
umesababisha Rais Dk.John Magufuli kutoa maelekezo kwa uongozi wa Wizara
ya Maji yakiwemo ya kuanza kuchunguzi kuanzia leo na kisha akabidhiwe
ripoti haraka huku walioshirikiana na mkandarasi wa mradi huo kula
fedha zaidi ya Sh. bilioni 200 kuanza kuzitapika fedha hizo.
Rais
Magufuli ametoa maelekezo na maagizo hayo leo wakati akihutubia
wananchi wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro wakati akiomba ridhaa ya
kuomba tena kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 mwaka huu ili
aendelee kuongoza nchi na kuiletea maendeleo.
Ametumia
nafasi hiyo kuwaomba wananchi hao msamaha kwa mradi huo kuchelewa
kukamilika kwani aliahidi kuutekeleza alipokuwa akiomba kura mwaka 2015
lakini cha kusikitisha hadi sasa haujakamilika ambapo amesema mradi wa
maji wa Bwawa la Mungu umeshindwa kukamilika mapema kwani ulitakiwa uwe
umekamilika mwaka 2017.
"Hadi
leo hii bado, sasa nasema hapa mkandarasi anayetekeleza, Waziri wa
Maji najua anasikia , ndani ya mwezi mmoja nataka abadilike aongeze
kasi ya kumaliza mradi huu nisipoona mabadiliko namfukuza huyo
mkandarasi.Haiwezekani wananchi wa Hedaru wazame kisa changamoto za maji
wanasubiri mradi huu kwa muda mrefu.
"Hivyo
nasema kwa dhati nawaomba radhi, huyo kandarasi huyu kama wapo
marafiki zake, watu wa Wizara ya Maji walikula naye waanze kuzitapika
hizo fedha kuanzia leo hii.Ndio maana siwezi kuzungumza uongom
ninafahamu kuzungumza uongo ni dhambi.
"Hivyo
iwe Waziri au Naibu ama Katibu na Mkurugenzi kwa sababu bado ni Rais
mpaka sasa,kesho waje wakague mradi na mkandarasi wake halafu nikifika
Moshi waniletee ripoti yake.Nawaombaradhi nimekosa sana,
nisamehe,"amesema Dk.Magufuli.
Hata
hivyo amesema anafahamu tatizo la mradi huo ni mkandarsi na kwamba
atalala nae mbele kwani haiwezekani Sh.bilioni 262 zilizotolea halafu
yeye acheze nazo wakati kazi hadi sasa kazi imefanyika kwa asilimia 64
tu na kama yupo eneo hilo la mkutano hata akimnyima kura hajali.
Wakati
akitoa maelekezo hayo Naibu Waziri wa Maji alikuwepo hapo na hivyo
amemtaka pamoja na watalaamu wake wa maji Same, Mkurugenzi wa Mkoa na
Wilaya wakae kutafuta ufumbuzi na maagizo yake yapo pale pale.
"Nasema
ukweli nitawafukuza wezi na ikiwezekana nitatoa amri awekwe ndani
mkandarasi kwani haiwezakani wapo watu waliokufa kwa kukosa maji. Kama
mlipata mkandarasi wa kughushi mwende mkatatue,haiwezekani nikawa Rais
halafu maji hayapo na kama ni fedha nilitoa tayari kakaeni mtafute
suluhu."
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...