Na Agness Francis, Michuzi Tv
MKUU wa Mkoa wa Dar es Saalam Aboubakar Kunenge ametembelea mradi wa KC land development plan inayotoa mikopo ya viwanja kwa muda mrefu bila riba,Uliopo kijiji cha Ngoma Mapinduzi halmashauri ya wilaya ya kigamboni Jijini Dar es Salaam, Sanjari na kuzindua visima vya maji safi na salama kwa wananchi hao waliikuwa na kiu ya huduma hiyo kwa muda mrefu.
Aidha baada ya khafla ya uzinduzi huo, Mkuu wa mko huyo akizungumza na vyombo vya habari pamoja na wakazi wa hapo ameipongeza kampuni ya KC land kuweza kutekeleza sera ya serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha inatengeneza mazingira bora ya uwekezaji ya kutoa fursa ya kufanya biashara kwa sekta binafsi.
Vilevile Kunenge amewataka wakazi wa Ngoma Mapinduzi kutovamia maeneo yaliotengwa na KC land kwa ajili yakujenga, Shule,Zahanati pamoja na nyumba za ibada.
“Niwaombe watendaji wa serikali za mitaa tusiruhusu sasa watu uvamia kujenga hovyo hovyo maeneo yalioachwa wazi, sehemu ya zahanati ibaki kuwa ya zahanati na nyumba za ibada pamoja na shule zibaki kuwa hivyo wazi.”Amesema RC Kunenge
Pia mkuu wa Mkoa huyo amewaahidi wakazi hao kuwa ataongea na talula kwa ajili ya ujenzi wa barabara ili kuhakikisha miundo mbinu inazidi kufika katika halmashauri hiyo ya wilaya ya Kigambioni.
Kwa upande wake mwenyekiti wa KC land development plan Khalid Mwinyi amesema kuwa mradi huo umejikita katika kutoa huduma kukopesha viwanja safi viliokwisha pimwa kwa mkopo wa muda mrefu usio na riba.
Mwenyekiti huyo amesema kuwa umuhimu wa kuwa na ardhi iliopimwa, vilevile amesema wameona wafanye pia utaratibu rafiki kuhakikiasha wanachi wanapata viwanja kwa bei nafuu ili kutimiza ndoto zao maana anaamini kila mtu anatamani kuwa na nymba bora ambapo mpaka sasa hekari 1500 zimesha gaiwa kwa wananchi hao kati ya 1800.
Mbali na hilo mweyekiti huyo amesema kuwa pia wanatoa huduma ya mikopo ya vifaa vya ujenzi kwa wateja hao.
“Tunao mradi wa ujenzi shirikishi ambapo tunatoa vifaa vya ujenzi ili kuwaondolea wananchi wetu ugumu wa kununua vifaa hivyo.” A mesema Mwinyi.”
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge akifanya zoezi la kuzindua kisima cha maji safi na salama ,ikiwa ni mradi uliofanywa na kampuni ya KC land development plan katika kijiji cha Ngoma Mapinduzi halmashauri ya wilaya ya Kigamboni Jijini Dar es salaam,Akisaidiana na mwenyekiti mtendaji wa KC land Khalid Mwinyi.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge akifungua bomba la maji katika uzinduzi huo wa kisima cha maji safi na salama Ngoma Mapinduzi Jijini Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...