Mkuu wa mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo (kulia) alipotembelea Uwanja wa nelson Mandela ili kujionea maandalizi ya uwanja huo kabla ya mechi baina ya Tanzania Prison na Simba SC tarehe 22.10.2020 pamoja naye ni Mhandisi Suleiman Mziray msimamizi wa ukarabati wa Uwanja huo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akisaidia kukata majani kwa mashine maalum ya kukatia majani alipotembelea kujionea maandalizi ya uwanja wa nelson Mandela kabla ya Mechi kali Oktoba 22, 2020.
Mmoja wa wafanyakazi wanaoendelea na kuupendezesha uwanja wa Nelson Mandela kwaajili ya mechi ya Tanzania Prison na Simba SC mjini Sumbawanga.

………………………………………………………

Wananchi mkoani Rukwa wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao ya Tanzania Proison inayotarajia kupambana na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom nchini Simba SC katika nyasi za Nelson Mandela Oktoba 22, 2020.

Hamasa hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipotembelea uwanja wa Nelson Mandela ili kujionea maandalizi ya uwanja huo kabla ya kupulizwa kipenga siku ya Alhamisi na kusema kuwa hakika ameridhishwa na maandalizi ya ndani ya uwanja nan je ya uwanja.

Mh. Wangabo alisema kuwa mashabiki siku zote wamekuwa ni mchezaji wa kumi na mbili ndani ya Uwanja na anategemewa kuongeza nguvu ya ushindi kwa kushangilia kwa nguvu zote katika dakika 90 za mchezo na kuongeza kuwa asingependa kuwaona wanarukwa wanaisahau timu yao ambayo imesababisha kuja kwa timu hizo nyingine zote na kushabikia timu ambazo ni wapita njia.

“Nisingependa kuona wanarukwa wanashabikia kwa wingi timu ya Simba, kwasababu timu ya simba ikishinda na nyingine ikaja ikashinda, na nyingine ikaja ikatushinda pia, timu hii itashuka daraja, itakaposhuka daraja hizi timu za Simba, Yanga, Azam na timu nyingine, hazitaonekana tena hapa kwahiyo tutakuwa hatujaitendea haki timu ya Prison, kwahiyo sisi tuishangilie timu yetu kwani hii ndiyo iliyotufanya Simba ije, Azam ikaja na Yanga itakuja na timu nyingine zitakuja,”

Aidha alisema kuwa anaiombea timu ya Tanzania Prison ushindi mbali na kutambua kuwa mpira una matokeo matatu, ya kushinda, kufungwa na sare na kusisitiza kwa washabiki wote wa mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi na kuwathibitishia kuimarika kwa usalama Pamoja na upatikanaji wa huduma zote muhimu kwa washabiki wataofika mjini Sumbawanga kutoka mikoa mimngine.

Kwa upnde wao mashabiki wa pande zote mbili wamejitokeza na kudai kila mmoja kuibuka na ushindi katika mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na wapenzi na wadau wa soka mjini Sumbawanga.

Mmoja wa mashabiki wa Tanzani Prison Patrick linus aliwatahadharisha wanasimba kuacha tabia ya kutembea na matokeo mifukoni na matokeo yake na wasifananishe Sumbawanga na maeneo mengi ambapo wameshakwenda na kuibuka na ushindi.

“’Game’ itakapochezwa Alhamisi, watachezea goli mbili lakini kwasababu ni watu wazima tutawapa nafasi ya kagoli kamoja tu, mi niwaombe tu wanarukwa, wakazi wa manispaa (ya Sumbawanga) tujitokeze kwa wingi, tuwape ‘Support’ Prison nao wafurahi, kamawalihama kutoka huko na kuja huku basi nasi tusiwaangushe,” Alisisitiza.

Naye Daudi Mbwala mshabiki wa timu ya Simba SC alisema kuwa Pamoja na kuikaribisha timu ya Simba na kuitakia ushindi lakini bado wanaiheshimu timu ya Tanzania Prison kwa kuweka makazi yake mjini Sumbawanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...