Na Jane Edward Michuzi TV,Arusha

Wanachama wa chama cha kuweka na kukopa cha Ngome Saccos wametakiwa kuendelea kuwa na imani na chama hicho huku wakiendelea kujijengea uwezo zaidi wa kuweka akiba.

Hayo yalisemwa jana mjini hapa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho,Brigedia Generali Omari Matteka wakati akizungumza  na waandishi wa habari kuhusiana  na chama hicho.

Brigedia Generali Matteka alisema kuwa, chama hicho kilisajiliwa rasmi mwaka 2007 na ni kati ya vyama vya kuweka na kukopa kongwe vilivyopo jijini Dar es Salaam  .

Aliongeza kuwa ,wanachama  wa chama hicho ni wanajeshi ,watumishi wa umma na wale waliostaafu katika wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa ambapo wana jumla ya wanachama 13,000 nchi nzima.

Brigedia Generali alisema kuwa ,wana  programu maalumu  ya kuwaandaa wastaafu ambapo hutoa mkopo kwao  miezi sita kabla pindi anapokaribia kustaafu  ili kufanya maandalizi mapema .

"kwa kweli Saccos yetu  tangu tumeanzisha tumeweza kuwakopesha wanachama wengi sana ambao wameona manufaa na matunda makubwa ya sacoss hii,na wameweza kuanzisha miradi mbalimbali "alisema Brigedia Generali.

Aliongeza kuwa,kwa mwezi wamekuwa wakikopesha wanachama wake  wastani wa  shs  3.8 bilioni.

Alifafanua zaidi kuwa,wanachama  wengi wameweza kufaidika na kuanzisha makazi Bora pamoja  na miradi mbalimbali ya maendeleo jambo ambalo limeleta mafanikiwa makubwa kwao.

Hata hivyo alitoa wito kwa wananchi mbalimbali kuzitumia vizuri vyama hivyo vya kuweka na kukopa kwani ni mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali sambamba na kuweza kuanzisha miradi .


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...