MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Dkt James
Mataragio  akizungumza na wachezaji wa timu za shirika hilo ambazo
zinashiriki kwenye michuano ya Shimuta inayoendelea kutimua vumbi kwenye
viwanja mbalimbali mjini hapa.

MKURUGENZI
Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Dkt James
Mataragio  kulia akiwa na Katibu wa Michezo wa Shirika hilo Elinaike
Naburi wakiwasikiliza watumishi wa shirika hilo ambao ni wanamichezo
wanaoshiriki mashindano ya Shimuta Jijini Tanga

Mmoja
wa wachezaji wa timu ya TPDC akichangia jambo wakati wa kikao hicho na
Mkurugenzi wa TPDC Dkt James Mataragio ambaye hayupo pichani

Mmoja wa wachezaji wa timu ya TPDC akichangia jambo wakati wa kikao
hicho na Mkurugenzi wa TPDC Dkt James Mataragio ambaye hayupo pichani

Sehemu
ya watumishi wa TPDC ambao wanashiriki mashindano ya Shimuta Jijini
Tanga wakimsikiliza Mkurugenzi wa Shirika hilo Dkt James Mataragio

Sehemu ya watumishi wa TPDC ambao wanashiriki mashindano ya Shimuta
Jijini Tanga wakimsikiliza Mkurugenzi wa Shirika hilo Dkt James
Mataragio

Mkurugenzi
wa Shirika hilo Dkt James
Mataragio  wa pili kutoka kushoto akiwa kwenye picha ua pamoja na
wachezaji wa timu za shirika hilo ambazo zinashiriki mashindano ya
Shimuta

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Dkt James Mataragio amesema wameyatumia mashindano ya Shimuta yanayoendelea Jijini Tanga kama njia ya kujitangaza hivyo yatakuwa na tija kwao kutokana na kwamba wamekuwa wakifanya biashara ya kuuza gesi na shughuli za kutafuta mafuta.

Dkt Mataragio aliyasema hayo leo jijini Tanga wakati akizungumza na wachezaji wa timu za shirika hilo ambazo zinashiriki kwenye michuano ya Shimuta inayoendelea kutimua vumbi kwenye viwanja mbalimbali mjini hapa.

Mkurugenzi huyo ambaye alifika Jijini Tanga leo asubuhi kushiriki katika timu yao inayoshiriki kwenye mashindano ya Shimuta amesema wamekuwa washiriki wazuri kwa miaka mingi.

Alisema kila siku Shirika hilo limekuwa na timu ya ushindi ambapo wamekuwa wakifanya hivyo katika mashindano mbalimbali huku akieleza mwaka huu wamekuwa mahiri kwa kuweza kuleta ushindani.

Aidha alisema umahiri huo umesaidia kuleta ushindani kwenye michezo mbalimbali kwa mfano mchezo wa Wavu,Kikapu,Riadhaa,Karata ,Pete na Mpira wa Miguu ambapo wameshiriki kote na kuweza kushinda vikombe sita na kupata medali moja lakini kikubwa zaidi wamejenga afya ya wafanyakazi wao.

“Ushiriki wetu umekuwa na umuhimu kwa sababu michezo ni afya na inaongeza tija kwa hiyo mimi kama Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC nalitambua hilo na ndio maana siku zote nawatia moyo vijana wetu kushiriki kwenye michezo kwa sababu najua michezo inaleta tija”Alisema

“Lakini kikubwa zaidi sisi kama TPDC ni shirika la Serikali ambalo linafanya biashara ya kuuza gesi na shughuli za kutafuta mafuta hivyo kushiriki kwenye michezo hiyo ni kuitangaza TPDC na shughuli ambazo tunazifanya “Alisema

Alisema kwa sababu wanatumia fedha nyingi kujitangaza lakini kwa vijana wao kushiriki kwenye michezo hiyo wanatangaza bidhaa zao kwa namna moja au nyengine kwa sababu wana kukutana na watu wengi kutokana na michezo huusisha watu wengi na wanajitangaza na kufahamika wanafanya nini na ni nani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...