Msanii wa Muziki wa R &B Behman Paul ' Ben Pol'

Na Mwandishi Wetu. Dar 

MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Flava Benham Paul 'Ben Pol' amewashukuru mashabiki wake kwa Kumpa ushirikiano kila anapotoa nyimbo yake mpya.

Ben Pol ameachia wimbo wake mpya ujulikanao kama Hiyo ndio Mbaya. 

Amesema amekuwa akipata ushirikiano kutoka kwa mashabiki wake hivyo ujio wa muziki wake huo mpya ambao ameutoa kwa staili ya Singeli.

"Nashukuru kwa sapoti ninayopata kutoka kwa mashabiki zangu na wadau , sasa nina miaka 10 kwenye muziki wamekuwa na mimi bega kwa bega, sasa nimekuja na wimbo katoka staili ya singeli unaitwa "Hiyo ndio Mbaya" 

Amesema wimbo huo amemshirikisha msanii mpya Tamimu, wa kiufanyia katika ya Pizzey Records, chini ya Mtayarishaji (Producer) Jay Stereo, 

"katika kuelekea kufunga mwaka nitatoa wimbo mpya kila wiki, mashabiki zangu wajiandae kupokea kazi zangu", amesema 

Pia amesema ameanza kuzunguka mikoani kufanya matamasha ya kuwashukuru mashabiki zake akianzia Mkoa wa Mbeya , mikoa mingine inafuata naomba wampokee.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...