Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akizungumza katika uzinduzi huo kulia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman wakati walipofafanua mambo mbalimbali kuhusu huduma hiyo kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki.

Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba (kushoto)  akizungumza jambo mara baada ya uzinduzi wa huduma za bima zitakazokuwa zikitolewa na benki hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akipongeza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman mara baada ya kuzindua huduma za bima za benki hiyo kwa ushirikiano na Kampuni ya Bima ya Sanlam ya jijini Dar es salaam kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba akifuatilia jambo wakati wa uzinduzi huo kulia ni  na Mkuu wa Wateja wa Kawaida wa Benki ya Standard Chartered nchini Tanzania Be.Ajmair Riaz.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman akielezea namna ushirikiano wa kampuni hiyo na benki ya Starndard Chatered zitakavyotolewa kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani.
Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akipongeza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman  mara baada ya kuzindua huduma za bima za benki hiyo kwa ushirikiano na Kampuni ya Bima ya Sanlam ya jijini Dar es salaam kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba  akizungumza jambo mara bmkatika uzinduzi wa huduma za bima zitakazokuwa zikitolewa na benki hiyo kulia ni Mkuu wa Wateja wa Kawaida Benki ya Starndard Chartered Bw Ajmair Riaz

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

KATIKA kuendelea kuwajali wateja katika kutoa huduma zao benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na kampuni ya Sanlam wamezindua huduma ya bima za bidhaa kwa wateja ili kuongeza thamani kwa wateja wao.

Uzinduzi huo wa bidhaa za bima uliokwenda kwa kauli mbiu ya "Tunavilinda vyenye Tija," umehusisha bidhaa mbalimbali ikiwemo nyumba na magari kwa ulinzi na usalama wa mali za wateja wao.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani amesema kuwa suala la bima limekuwa na manufaa kwa sasa kutokana na ulinzi na usalama kupitia bima za bidhaa mbalimbali ikiwemo magari, nyumba na afya.

Amesema Tanzania ni sehemu salama na  Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Joseph Magufuli imekuwa ikishirikiana kwa karibu na sekta binafsi katika kujenga uchumi wa Taifa.

"Bima ina umuhimu mkubwa hasa katika ulinzi na usalama, watanzania lazima waelewe umuhimu wa  kukata bima katika mabenki kwa manufaa yao binafsi na mali zao."

Amesema kuwa huo ni ushirikiano wa kibiashara kwa maendeleo ya jamii na taifa la Tanzania na kuahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano kwa kuendeleza bima zikiwemo za sekta ya madini na afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman mabenki kuanza kuuza bima ni muhimu kwa kuwa wanafahamu ni nini mteja anacho na anachoweza kununua.

Amesema kuwa Kampuni hiyo iliyotimiza miaka 102 tangu kuanzishwa kwake ina malengo ya kufikia asilimia 50 ya watanzania wanaomiliki bima hadi kufikia mwaka 2030, na bima hizo zikiwa ni pamoja na bima za nyumba na magari.

Vilevile amesema, Sanlam imekuwa nchini kwa miaka 20, wakiwa katika nchi 44 zikiwemo nchi zote za Afrika Mashariki na kuahidi kuendelea kutoa huduma  bora kwa ustawi wa jamii na taifa la Tanzania.

Amesema kuwa watanzania wachukue bidhaa za bima kutoka Standard Chartered kwa kuwa wanavilinda vyenye tija.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...