Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Corporation Waziri Kindamba akizungumza na wananchi wa kijiji cha Isuli katika uzinduzi wa mnara wa mawasiliano wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora.

       Wananchi wa kijiji cha Isuli, wilayani Uyui mkoa wa Tabora walijitokeza kwa wingi  katika uzinduzi wa Mnara wa Mawasiliano kijijini hapo. 

Wananchi wa kijiji cha Isuli wakifanya usajili wa laini za simu za TTCL Corporation katika hafla ya uzinduzi wa mnara wa mawasiliano uliofanyika katiko kijiji hicho, wilayani Uyui mkoa wa Tabora. 

  Mbunge wa Jimbo la Igalula Venant Daudi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Isuli katika hafla ya uzinduzi wa mnara wa mawasiliano kijijini hapo. 

 Mkuu wa  Wilaya ya Uyui Gift Msuya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Tabora akihutubia wakazi wa kijiji cha Isuli katika uzinduzi wa mnara wa mawasiliano wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora. 

 Mkuu wa  Wilaya ya Uyui Gift Msuya, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Corporation Waziri Kindamba, Mbunge wa Jimbo la Igalula Mhe. Mhe. Venant Daudi, Diwani wa Kata ya Kizengi  Mhe. Magidinga Masaga na viongozi wa serikali ya kijiji wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa mnara wa mawasiliano katika kijiji cha Isuli, wilayani Uyui, mkoa wa Tabora. 

1.  Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Corporation Waziri Kindamba akitoa maelezo kwa Mgeni Rasmi na Mkuu Wilaya ya Uyui  Gift Msuya  kuhusu mitambo ya mawasiliano iliyofungwa katika kijiji hicho kwenye uzunduzi wa Mnara wa mawasiliano, kijijini Isuli, wilayani Uyui, mkoa wa Tabora.

1 Diwani wa Kata ya Kizengi  Mhe. Magidinga Masaga akizungumza na wananchi wa kijiji cha Isuli katika hafla ya uzinduzi wa mnara wa mawasiliano kijijini hapo.


MKUU wa Wilaya ya Uyui Gift Msuya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Tabora amezindua mnara wa mawasiliano katika kata ya Kizengi, kijiji cha Isuli wilayani Uyui na kuwataka wananchi kutumia mawasiliano kwa ajili ya kulinda usalama na kukuza maendeleo ya Taifa letu.

Akizindua mnara huo,  Gift Msuya amesema mawasiliano ni muhimu sana katika kulinda usalama na kukuza uchumi wa Taifa letu.

“Nawasihi  wananchi wa Isuli kutumia mawasiliano kwa ajili ya kukuza uchumi wa Taifa letu kwa kuwekeza zaidi katika kutafuta masoko na fursa mbalimbali ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.” amesema Mkuu wa Wilaya huyo.

Amesema wakazi wa kijiji cha Isuli wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo vya Usalama ili sheria ichukue mkondo wake kwa wote watakaohujumu miundombinu ya mawasiliano. Pia amesitiza kuwa wananchi wasikubali kuona watu wachache wenye malengo yao binafsi wanaharibu uwekezaji kama huu ambao Serikali imewekeza kwa nguvu nyingi ya kuwapatia wananchi mawasiliano.  

Aidha, Mkuu wa Wilaya ameipongeza Shirika kwa kufanikisha kupeleka mawasiliano ya simu kwenye  vijiji vya  Alex- Uyui, Buhekela- Igunga, Nsenda Mlimani-Urambo, Isuli- Uyui, Shilla- Nzega, Nsogoro-Urambo, Usunga- Sikonge, Malagano -Igunga na vijiji vingine vya Ngulu Mpakani-Igunga, Igoweko-Uyui, Nyaua-Uyui na Magua-Sikonge ambapo ujenzi  wa minara unaendelea.

Aidha, Mkurugenzi  Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania Waziri Kindamba amewataka wananchi wa kijiji cha Isuli kuhakikisha miundombinu ya mnara huo wa mawasiliano na miundombinu mingine ya Shirika la Mawasiliano Tanzania, inalindwa dhidi ya wahalifu. 

“ni jukumu letu sote, tushirikiane kwa pamoja, uongozi wa Kata, wananchi pamoja na Kamati ya ulinzi na usalama katika kulinda miundombinu hii ya mawasiliano.” amesema Mkurugenzi Mkuu.

Aidha, Kindamba ametoa rai kwa wananchi  kutumia huduma  za vifurushi ambavyo ni vya gharama nafuu,  pia kuwataka wananchi kuchangamkia fursa za kujiongezea kipato kwa kuwa mawakala wa kuuza vocha na mawakala wa T-PESA.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu amesema kuwa Shirika litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali  katika kutekeleza mikakati na mipango mbalimbali ya kupeleka huduma za mawasiliano maeneo ambayo bado yana changamoto ya mawasiliano hasa maeneo ya vijijini na pembezoni mwa mipaka ya nchi yetu.

Akizungumza na wananchi katika tukio hilo, Mbunge wa Jimbo la Igalula,  Venant Daudi ameishukuru Shirika la Mawasiliano Tanzania kwa kupeleka huduma ya mawasiliano katika kijiji cha Isuli,na kusema  uwepo wa mawasiliano katika kiijiji kutaondoa kero ya wananchi ya muda mrefu ya kukosa huduma za mawasiliano.

Aidha,  Mbunge huyo ametumia fursa hiyo kumuomba Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano kumsaidia kutatua changamoto za mawasiliano kwenye vijiji vingine ambavyo havina huduma za mawasiliano katika  jimbo la Igalula Wilayani Uyui, Tabora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...