Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge amewataka wananchi wa Mkoa huo kuhakikisha kila Jumamos wanafanya zoezi la usafi wa mazingira kuanzia saa 12 Asubuhi hadi saa tatu ili kujikinga na magonjwa ya Mlipuko na kuliweka jiji kuwa Safi.

RC Kunenge ametoa maelekezo hayo wakati alipokuwa anazungumzia zoezi la usafi linalotaraji kufanyika Jumamosi ya Disemba 05 ambapo amesema Mkoa umejipanga vizuri kuhakikisha magari ya kubeba taka yanakuwa ya kutosha kwenye kila maeneo.

Aidha RC Kunenge amewaelekeza Wakuu wa Wilaya za Jiji hilo kuhakikisha wanasimamia usafi Katika maeneo yao na kuhakikisha suala la usafi linazingatiwa na kila mmoja.

Pamoja na hayo RC Kunenge ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo kuhakikisha suala la usafi linakuwa sehemu ya maisha yao na sio kusubiri kushurutishwa na Sheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...