Ubalozi wa Tanzania Qatar ukishirikiana na Wanadiaspora kutoka Tanzania unashiriki kwenye Tamasha la Kumi la Kiasili la Majahazi lijulikanalo kama 10th Katara Traditional Dhow Festival.Tamasha hilo  linafanyika Doha kuanzia tarehe 1-5 Disemba 2020 ambapo Tanzania inaelezea utamaduni wa kiasili wa jahazi wa mwambao wa Afrika Mashariki na Zanzibar ambapo ndio kitovu cha utamaduni huo. 

Utamaduni huo ulipelekea kuibuka muingiliano wa utamaduni wa lugha, mavazi, chakula na dini pamoja na matumizi ya Majahazi. Ubalozi umepata fursa pia ya kutangaza bidhaa za kitanzania kama viungo(spices) asali, korosho na kahawa pamoja na kutangaza utalii wetu. 

Mgeni Rasmi, Mhe. Hamad bin Abdulaziz Al Kawari, Waziri wa Nchi na Mkurugenzi wa Maktaba ya Taifa pamoja na Meneja Mkuu wa kijiji hicho cha Katara, Dr. Khalid bin Ibrahim Al Sulaiti  wakipata maelezo kwenye banda la Tanzania walipotembelea wakati wa uzinduzi wa Tamasha hilo.

Mabalozi wa Nchi za Afrika Mashariki waliopo Qatar wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Banda la Maonesho la Tanzania

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...