Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John Magufuli pamoja na Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Mwinyi, katika Ikulu ndogo ya Chato Mkoa wa Geita.

Maalim Seif amefika mapema leo asubuhi tarehehe 14/01/2021, katika uwanja wa ndege wa Mwanza  na kupokelewa na Viongozi waandamizi wa Kiserikali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza Mh. Sevelin Lalika.

Maalim Seif alipata fursa ya kutembelea ujenzi wa Daraja la Magufuli lililopo Kigongo feri Mpakani mwa Misungwi na Sengerema.

Mradi wa daraja hilo ukikamilika utaleta mafanikio makubwa ya kuunganisha baadhi mikoa ya Tanzania pamoja na kuunganisha Tanzania na Nchi jirani kama Burudi,Rwanda na Congo.

Baada ya Ziara hio Maalim Seif alifika Chato kwenda kukutana na Marais hao ambao walijadili mambo mengi na baadae kuzungumza na umma wa Watazaznia na Dunia kwa Ujumla kupitia waandishi wa habari.

Katika mkutano na waandishi wa habari Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar alisema;

”Tumebadilishana mawazo juu ya mustakbali wetu wa Zanzibar na namna bora zaidi ambavyo tunaweza kuwatumikia Watanzania”.

Katika kusisitiza hilo Makamu wa kwanza amesisitiza yakwamba;

"Kwanamna tulivyo zungumza na kukubaliana inaonesha wazi Rais Magufuli anania njema ya kutuunga mkono na kuyaboresha maisha ya Wazanzibar wa kisiwa cha Pemba na Unguja".








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...