Charles James, Michuzi TV

Kamati ya LAAC imeteuliwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, na leo hii wajumbe wa kamati hiyo wameanza kupewa mafunzo ya wiki moja ya kuwajengea uwezo ili waweze kusimamia matumizi ya rasilimali za umma zinazopelekwa kwenye Halmashauri zetu zote 185 Tanzania.

Akizungumza jijini Dodoma Makamu Mwenyekiti wa LAAC ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukene, Selemani Zedi amesema watayatumia mafunzo hayo kikamilifu katika kuwatumikia watanzania

" Kwa mujibu wa majukumu yetu kikanuni, tutahakikisha rasilimali za umma zinazopelekwa halmashauri zinatumika kama zilivyokusudiwa, na matumizi yote yanafanyika kwa mujibu wa sheria ya fedha ya Serikali za Mitaa.

Kama ambavyo tuliapa kuilinda Katiba yetu na kuwaahidi wananchi wetu kuwatumikia kwa nguvu zetu ndivyo tutakavyozilinda rasilimali zetu kwa wivu mkubwa," Amesema Mbunge Zedi.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...