TAARIFA KWA UMMA KIKAO CHA WAZIRI WA KILIMO NA MAAFISA KILIMO WA MIKOA NA HALMASHAURI

Dodoma, 27 Januari 2021

Wizara ya Kilimo imeandaa kikao kazi cha Waziri wa Kilimo na Maafisa Kilimo wa Mikoa na Halmashauri nchini kwa lengo la kujadili changamoto za upatikanaji huduma za ugani na nini kifanyike kuwasaidia wakulima kuboresha kilimo ili kiwe na tija.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) imesema kikao hicho kitajadili na kuweka mikakati ya utekelezaji wa kuhakikisha wizara inaleta mapinduzi makubwa na kukifanya kilimo kuwa cha kisasa na chenye faida kwa mkulima kwa kuzingatia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II).

Mkutano huo utafanyika tarehe 29-30 Januari ,2021 katika ukumbi wa Mikutano wa LAPF Jijini Dodoma kuanzia saa 3.00 asubuhi.Katika kikao hicho Wizara itaelezea vipaumbele na mwelekeo wake katika kipindi cha miaka mitano ijayo  (2020-2025).

Imetolewa na;

Gerald M. Kusaya

KATIBU MKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...