NA Neema Mbuja, Rukwa

Shirika la umeme Tanzania TANESCO kupitia Idara ya masoko imeendelea na kampeni ya kutoa Elimu kwa wamiliki wa viwanda,machimbo ya madini, na mashine za kusaga kwa mkoa wa Rukwa ili kuwapatia Elimu juu ya matumizi Bora ya umeme sanjari na kukagua miundo mbinu ya umeme pamoja na mota zinazotumiwa kwenye kuendesha mashine viwandani

Miongoni mwa Elimu wanayopatiwa Ni pamoja na namna ya kutumia vifaa ambavyo vinatumia umeme kidogo, umuhimu wa kukagua mota zao Mara kwa Mara kwa ajili ya kuleta ufanisi na Usalama wa miundo mbinu ya TANESCO kwenye maeneo yao

Akizungumza na wamiliki wa viwanda kwenye Wilaya za Sumbawanga mjini na Laela , mhandisi kutoka  kutoka idara ya utafiti Baraka Kanyika  amesema kuwa kwa Sasa baadhi ya  viwanda vinatambua umuhimu wa kufunga power factor ingawa baadhi bado hawajatambua

Kuhusu wamiliki wa mashine  za kusaga Kijiji Cha muze Wilaya ya Laela mkoa wa Rukwa mhandisi Kanyika ameshauri kuendelea kuwapatia Elimu ya umuhimu wa kukagua mota zinazoendesha mashine zao Mara kwa Mara ili kuziongezea ufanisi wa utendaji kàzi na kulinda miundo mbinu ya shirika.









<

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...