Picha ya pamoja ya waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya siku moja yaliyoandaliwa na yaliyohusu Afya ya Uzazi kwa vijana yaliyofanyika jijini Arusha.
Waziri Njau ni mratibu wa shirika Shirika lisilo la kiserikali la japaygo akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya Siku moja yaliyofanyika Jijini Arusha katika Hospital ya mount Meru
Dkt.Mratibu wa Afya ya akili katika ngazi ya mkoa akizungumza na waandishi wa habari juu ya Afya ya Akili na changamoto wanazopitia vijana.

Mratibu wa  mkoa wa Arusha Afya ya mama na mtoto Belinda Mumbuli akizungumza na waandishi wa habari katika semina ya siku moja  Jijini Arusha

WANAHABARI TUMIENI MAJUKWAA YENU VYEMA KUTOA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA

Na.Vero Ignatus,Arusha.

Shirika lisilo la kiserikali la Jhpiego chini ya mradi wake wa ''Tupange Pamoja'' kwa  kushirikiana na hospitali ya mkoa ya Arusha,wameendeska mafunzo ya siku moja kwa kwa waandishi wa Habari, lengo kuu likiwa ni kujadi juu ya Afya ya uzazi kwa vijana ,kwani wao wana uwanja mpana wa kutoa elimu

Waziri Njau ni Mratibu wa mkoa wa shirika hilo ,amesema kuwa jamii haswa vijana bado hawana uelewa mkubwa juu ya  Afya ya uzazi,hivyo vijana wana changamoto kubwa,kwani huduma Rafiki kwa vijana  hao bado haijaeleweka katika jamii

Amesema vijana wengi wanamatatizo ya Afya ya akili ,dawa za kulevya,matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango ni yapo chini kwa vijana wale ambao wameshapata ujauzito,hivyo wameomba vyombo vya habari viweze kutumika vyema ili vijana waweze kupata habari.

Amesema kuwa wanataka kila mwandishi wa habari apate huduma rafiki kwa vijana ,ili waweze kuitoa kwa namna ya kipekee, Jambo ambalo litasaidia vijana wengi kuelimika,sambamba na  kupunguza Mimba za utotoni,kuwajengea Afya bora ,kwani hata Mimba nyingi zinazoharibika,vifo vingi vitokanavyo na uzazi vimekuwa vikiwapata vijana zaidi ,pamoja na watoto wanaozaliwa wanaliwa ni njiti.

''Kikubwa kila kijana anabaguliwa,anaonekana kwa kiasi kikubwa siyo mwadilifu ,na hata akipata tatizo lolote la Afya ya uzazi ni Kama vile amejitakia mwenyewe, kwahiyo inakuwa Kama vile ni laana,hivyo anaambiwa acha tumuone'' .Alisema Njau

Amesema kuwa kumuhudumia kijana lazima kuwe na suala zima la usiri na faragha kutampelekea kijana kujiona yupo salama,kwani wanahitajika kupata huduma zote na siyo baadhi, hivyo itanisaidia kuondoa ule ubaguzi na Kujinyanyapaa 

Dkt.Charles Migunga ni Mratibu wa Afya ya Akili katika ngazi ya mkoa amesema kuwa, vijana wengi wamekuwa wakijiingiza kwenye mambo yasiyofaa kutokana na changamoto mbalimbali za kimaisha ,hivyo waandishi wa habari wanapaswa kupaza sauti ili kuwanasua kutoka katika matendo hayo ,kama utumiaji wa dawa za kulevya, pamoja na kuwahabarisha kuhusu elimu ya Uzazi.

Dkt.Migunga amesema kuwa hadi sasa wameweza kuzunguka katika halmashauri ya jiji Arusha,Meru,na Arusha Dc katika shu le kadhaa za sekondari na msingi ambapo vijana kuanzia darasa la 5,6 na darasa la 7 wachache baadhi yao wameshaanza kutumia bangi,pombe mirungi, ugoro na wengine wanatumia gundi

Migunga aliongeza kuwa  hali kwa jiji la Arusha siyo nzuri sana kwa vijana hao wa shule za msingi na sekondari,hivyo wamechukua jukumu la kuwaelimisha waalimu wa Afya,kwa kuwapatia masomo na mada ili waweze kufundisha.

Kwa upande wake Mratibu   wa mkoa wa Arusha Afya ya mama na mtoto Belinda Mumbuli alisema kuwa Afya ya uzazi ina mapana yake, pia uzazi wa mpango ukiwemo ndani yake,hivyo changamoto nyingi wananzokutana nazo wasichana wakiwemo shuleni, ni kupoteza mwelekeo wa elimu kwani akipata ujauzito akiwa shuleni anafukuzwa.

''Anapopata mimba siyo wazazi wote wapo tayari kuishi nae nyumbani ,bali wengine watasababisha msichana huyu kuolewa katika umri mdogo hajui hili wala lile, mwisho wa siku anapata madhara maungo yake hayajakomaa,wakati wa kujifungua anapata shida wengine wanaambiwa wakazalie kwa wakunga wa jadi' inatokea shida ya kupoteza maisha aidha mama au mtoto ama tunawapoteza wote''Alisema Belinda.

Amesema changamoto nyingine kubwa wanayopitia wasichana ni kutengwa,pamoja na mtoto kukosa mahitaji muhimu,ama wakati mwingine kwa vile amepata ujauzito na hataki wazazi wafahamu anaichokonoa ,jambo amabalo linampelekea kupata matatizo, hivyo amewaomba waandishi wa habari kushirikiana kwa pamoja ili kuwaokoa vijana katika changamoto ambazo zinazowakumba juu ya Afya ya uzazi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...