Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt.
Hassan Abbasi, amesema Maelekezo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu
utoaji wa habari za Serikali kwa umma yanatekelezwa kwa kasi na ofisi
au mtendaji yeyote wa ofisi ya umma atakayekaidi asitafute wa kumlaumu.
“Waziri wa Habari Mhe Innocent
Bashungwa, hivi ninavyoongea hapa ameshasaini barua yenye maelekezo hayo
na zaidi kuzijulisha taasisi zote za umma nchini kuhusu tathmini
itakayofanyika,” alisema.
Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo
mkoani Morogoro wakati akitoa mada kwenye semina ya wahariri kuhusu
Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere.
Amesema utoaji wa habari kwa
umma ni jambo la kisheria na kikatiba hivyo hata maelekezo ya Rais yako
sahihi na atakayekaidi “amekaidi mamlaka, amekaidi sheria na amekaidi
katiba.”
Katika hatua nyingine, Dkt.
Abbasi amewataka wahariri na waandishi nchini kuenzi misingi ya weledi
na uzalendo katika kazi zao ikiwemo kufanya utafiti kwanza kuliko
“kufakamia” mawazo na maoni ya watu wasioitakia nchi mema.
“Baadhi ya waandishi hawafanyi
utafiti wala kutaka kujua mambo kwa kina na huishi wakifakamia tu kila
kinachosemwa na mabeberu kupinga maendeleo yetu. We mwandishi gani sisi
ndio Serikali na ndio wenye hela na ndio wenye mradi tunakwambia
tunakwenda kujenga mradi Rufiji, anatokea wakala wa mabeberu mmoja
kashiba mivyakula ya kwenye kopo huko anakofadhiliwa kuishi anakwambia
huo mradi hautajengwa, hawana hela hao, mwandishi unatoka unamwamini
wakala wa beberu unaandika na kusambaza uongo, we vipi mbona hatukuelewi
na wewe ni wa moto au wa baridi?” alihoji Dkt. Abbasi akisisitiza tangu
utekelezaji wa mradi wa Umeme JNHPP Rufiji uanze hakuna malipo ambayo
Serikali imechelewesha au kushindwa kuwalipa wakandarasi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...