Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo na Mbunge wa jimbo la Mkuranga,Abdallah Ulega ametoa mifuko 340 ya saruji pamoja na Fedha taslimu zaidi ya milioni nne na Mabati 30 za kuanzishia ujenzi wa shule za Msingi na Sekondari pamoja na Zahanati katika kata za Vianzi,Mipeko,Nyamato na Kimanzichana
Shule hizo alizozichangia ni shule ya msingi Kisima inayojengwa kata ya Vianzi shule ya msingi Kisiwani inayoanzishwa katika kata ya Mipeko Shule ya Sekondari ya kata ya Kimazichana Shule ya msingi kijiji cha Mkiu kata ya Nyamato, Zahanati ya kimanzichana Magharibi na Zahanati ya kimazichana Kaskazini Wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
Akizungumza na wanachi wakata hizo kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake ya kutoa shukrani kwa wananchi pamoja na kukagua miradi ya maendeleo aliyoifanya hapo jana katika kata hizo nne,Ulega amesema hatua ya ujenzi huo umekuja kutokana na changamoto ya mrundikano wa wanafunzi madarasani pamoja na umbali mrefu wanaotembea wanafunzi kufuata elimu.
"Wanafunzi wanatembea umbali wa zaidi ya kilomita 5 kufuata shule,wanavuka mito,kiukweli wanakutana na changamoto nyingi zinazohatarisha maisha yao hali inayowapa hofu wazazi,hivyo kukamilika kwa shule hizo kutapunguza changamoto kwa kiasi kikubwa katika maeneo husika". Amesema Ulega.
Aidha Ulega pamoja na kutoa mifuko ya saruji na pesa taslimu pia ameshiriki kuchimba msingi wa ujenzi wa shule ya msingi Kisiwani kata ya Mipeko kwa kushirikiana na wananchi pamoja na diwani wakata hiyo,Adili Kinyenga ili kuendelea kuhamasisha maendeleo Mkuranga.
Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujitolea kwa hali na Mali na kuwaahidi kuendelea kuwaunga mkono ilikufanikisha ujenzi wa shule hizo,ili kutatua changamoto za kielimu Mkuranga.
Kwa upande wa madiwani wa kata hizo wakiwakilishwa na diwani wa kata ya Mipeko,Adili kinyenga amemshukuru Mbunge wa jimbo kwa juhudi zake za kusaidia wananchi na kuahidi kuisimamia shule pamoja na zahanati zinakamilika kwa wakati.
Sanjari na hayo Ulega ametembelea daraja la Mipeko na kumtaka diwani,kwa kushirikiana na wananchi kuona namna ya kupatikana kwa kivuko cha muda kabla ya mvua za masika kuanza kitakachowezesha wananchi kuvuka wakati serikali ikipambana kupatikana kwa daraja la kudumu katika eneo hilo.
Hata hivyo hapo awali serikali ilishatumia kiasi cha shilingi milioni 200 kujenga daraja katika eneo hilo kabla mvua kubwa za mwaka Jana kuliharibu,hivyo Ulega amesema yupo tayari kushirikiana na wananchi pamoja na diwani kuhakikisha kivuko cha muda kinapatikana ilikuondoa adha kwa wananchi wa kata ya mipeko.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...