KAMPENI ya MastaBata Sio Kikawaida iliyoendeshwa na Benki ya NMB imefikia tamati leo na jumla ya washindi 12 wamepatikana huku kila mmoja akijinyakulia zawadi yenye thamani ya shilingi milioni nane.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuwapata washindi hao, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa amesema katika fainali ya kampeni hiyo wateja hao wamepata nafasi ya kuchagua zawadi mbili ambazo ni kutembelea vivutio vya ndani vya utalii vya Serengeti, Ngorongoro na visiwa vya Zanzibar pamoja na bidhaa za nyumbani ikiwemo TV inchi 50 iliyounganishwa na kifurushi kwa miezi mitatu, jokofu la kisasa la milango miwili, kompyuta mpakato iliyounganishwa na printa, simu janja (Samsung A70,) water dispenser pamoja na Microwave.
Benki ya NMB bado inaendealea na kampeni kabambe katika kuhakikisha wateja wao wananufaika na kwa sasa wapo na kampeni ya 'Bonge la Mpango' ambayo wateja watapata nafasi ya kushinda pesa, bajaji na gari jipya aina ya Fortune lenye thamani ya shilingi milioni 165 katika Grand finale.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...