Mkurugenzi wa maziwa ya Asas Ahmed Salim Abri akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Lipuli na Bajaji 

…………………………………………………………………..

NA DENIS MLOWE, IRINGA

MKURUGENZI wa uzalishaji wa kampuni ya maziwa ya Asas, Ahmed Salim Abri, ameahidi kuwalipia mashabiki 100 kutoka umoja wa madereva Bajaji mkoa wa Iringa kuingia katika mchezo wa ligi soka daraja la kwanza Kati ya Lipuli Fc dhidi ya Kengold unaotarajiwa kupigwa katika uwanja wa Samora hivi karibuni.
 
Lengo la kuwalipia tiketi hizo ni kuwahamasisha wananchi wa mkoa wa Iringa kurudisha ushabiki wa soka na kuipa hamasa timu ya Lipuli kuibuka kidedea katika mchezo huo na kufanikisha lengo la kuirudisha ligi kuu soka Tanzania bara.Ahadi hiyo aliitoa wakati wa mchezo wa kirafiki Kati ya Lipuli fc na Bajaji FC ambapo Lipuli iliibuka na ushindi wa magoli 4 – 1 ukiwa na lengo la kuu la kujenga mahusiano kati ya madereva Bajaji na timu ya Lipuli.
Akiongea katika ufunguzi wa Mchezo huu Ahmed Salim  ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwa lengo ni kurudisha hamasa ya mchezo wa soka mkoani hapa ambapo ulipotea mara baada ya timu kushuka daraja 
 
Kutokana na Hilo atahakikisha wanarejesha hamasa ya mashabiki kuingia uwanjani ambapo kwa kuanza atawalipia madereva bajaji tiketi 1000 kwenye mchezo wa Lipuli dhidi ya Kengold.
“Kwa kutambua umuhimu wa mashabiki kwenye mchezo huo muhimu ambapo tunaamini uwepo wao utakuwa chachu ya mafanikio kwenye mchezo huo na kuwapa Nguvu wachezaji waibuke na ushindi na kuelewa kwamba Wana Iringa wako nyuma yao”Alisema
 
Nao viongozi wa Bajaji , Merab Kihwele akiwa sambamba na katibu wake ndugu Bryson wameahidi kuendeleza uhusiano ambapo wameuanzisha na pia wameahidi kuwa endapo Lipuli itaibuka kidedea watawanunulia mbuzi wachezaji ili wale kama sehemu ya pongezi.
Aidha wameahidi kuwa sehemu kubwa ya hamasa huku wakitumia vyombo vyao vya usafiri kuhamasisha abiria wengine kufika uwanjani kuwashangilia Lipuli.
 
Kwa upande wao uongozi wa Lipuli fc  wmeahidi kuulinda na kuuendeleza urafiki huu huku wakiamini kuwa hawa ni sehemu ya kundi muhimu ambalo litatutasaidia sana kwenye mipango yetu ya kuipandisha timu. 
 
Aidha wamemshukuru mkurugenzi Ahmed Salim Abri kwa kuwapa hamasa madereva bajaji na kushukuru viongozi wa bajaji na madereva wa bajaji kwa kukubali kuwa wamoja katika lengo la kuipandisha timu.Wakati huo huo mmoja ya wakurugenzi wa kampuni ya Asas,

Feisal Abri ametoa kiasi cha shilingi 400000/= kwa ajili ya kununulia jezi za Mazoezi kwa timu yetu ya Lipuli.

Uongozi wa Lipuli FC unapenda kumpongeza sana Feisal kwa mchango wake huo kwani umekuja wakati muafaka ambapo timu ilikuwa inauhitaji sana na jezi za Mazoezi. 
“Uongozi unatoa shukrani za dhati kwa ndugu Faisal kwani licha ya msaada wa leo lakini pia amekuwa mtoaji wa mara kwa mara kwenye klabu yetu na amekuwa mwepesi kila anapoombwa kuisaidia timu” 
 
Aidha klabu inapenda kuwakumbusha na wengine kuichangia timu yetu kwani inauhitaji mkubwa sana. Kipindi hiki ni kipindi ambacho tunatakiwa kuiandaa sana timu hivyo fedha nyingi zinahitajika kwahiyo tunatoa wito kwa wadau mbalimbali kuiunga mkono timu ili hatimaye tuweze kupanda Daraja kama ilivyo matarajio. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...