NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
CHAMA
Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimetoa cheti cha pongezi kwa Rais Dk
John Magufuli kwa kufanikisha ushindi wa chama hicho kushika dola,kwa
kipindi kingine cha miaka mitano.
Aidha cheti kingine kilitolewa kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete ambacho alikabidhiwa kabla ya mkutano huo.
Zawadi
hiyo kwa Rais na aliyekuwa katibu wa CCM Taifa Dk Bashiru Ally Kakurwa
ambaye ilikabidhiwa na mwenyekiti wa Ccm mkoa Ramadhan Maneno kwa mlezi
wa chama hicho Mkoa wa Pwani Gaudencia Kabaka wakati kikao maalum cha
Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.
Watu
wengine waliopewa vyeti vya shukrani ni pamoja na wabunge wa mkoa huo
na wale waliogombea nafasi hiyo, mkuu wa mkoa, wakuu wa wilaya,
wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa huo, wenueviti wa CCM wilaya za Mkoa
huo na wadau waliokiwezesha chama kushinda nafasi za urais, ubunge na
udiwani.
Akizungumza
kwenye kikao hicho mlezi wa Ccm Mkoa wa Pwani ,Gaudencia Kabaka alisema
kuwa licha ya changamoto iliyojitokeza ya utaratibu wa kadi za
kieletroniki kutokamilika wawatambue wanachama kwa kadi za zamani.
"Ukosefu
wa kadi za kieletroniki isisababishe mambo mengine yasiendelee kwani
zoezi hilo litakamilika hivyo msiwe na wasiwasi juu ya kadi hizo za
kisasa," alisema Kabaka.
"Tuwe
wavumilivu chama kiko vizuri na tunaelekea vyema na tunamshukuru Rais
kwa kuhakikisha nchi inakwenda na kuwaletea maendeleo wananchi," alisema
Kabaka.
Naye
mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Ramadhan Maneno alieleza,kumekuwa na
changamoto mara uchaguzi unapokwisha kutokana na makundi ya wagombea na
kusababisha mitafaruku ya hapa na pale.
Naye
Katibu wa Ccm mkoa wa Pwani Elia Mpanda akizungumzia juu ya kadi hizo
za kieletroniki alisema taratibu zinaenda vizuri hivyo wanaccm na
viongozi wasiwe na hofu.
Mpanda alisema ,teknolojia ina changamoto zake lakini haitasababisha kurudi nyuma katika mchakato wa kwenda kisasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...