Pendekezo hilo limewasilishwa na Katib Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao.
“Sisi kama Tanzania tumependekeza suala la lugha ya Kiswahili kutoka kwenye lugha ya kazi kwenye ngazi ya baraza la mawaziri hadi wakuu wa nchi na serikali wa SADC linabadilika na kuiwezesha lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi kwenye utendaji wa SADC,” Amesema Balozi Ibuge.
Balozi Ibuge ameongeza kuwa, SADC wamekuwa wakitumia lugha za kikoloni kwa muda mrefu na kwa busara za wakuu wa nchi na Serikali wameamua kuanza kwa mpangilio ambapo lugha ya Kiswahili itaanza kutumika katika ngazi ya baraza la mawaziri pamoja na vikao vya wakuu wa nchi, na kuishusha lugha hiyo kwenye sekta na kuingia rasmi katika matumizi ya SADC.
Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC unaotegemewa kufanyika tarehe 12, Machi jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao.
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...