Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Gisela Mugumira (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Agatha Madalle (kulia) wakijadiliana jambo na baadhi ya wajumbe wa TUGHE wakati wa zoezi la upandaji miti katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma kwa ajili ya kutunza mazingira ikiwa ni maandalizi ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani.

Afisa Tawala wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Haika Mlay na Mjumbe wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) wa wizara hiyo, Bi. Husna Hamis wakishirikiana kupanda mti katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani.

Baadhi ya wajumbe wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Wizara ya Fedha na Mipango wakipeleka miti katika eneo la upandaji katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma kuelekea sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani.


Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Gisela Mugumira akipanda mti katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yanayotarajiwa kufanyika Machi 8, 2021.

Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Agatha Madalle akisawazisha udongo baada ya kupanda mti katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yenye kaulimbiu ya “Wanawake katika uongozi chachu kufikia Dunia yenye usawa”.

 

Wajumbe wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Wizara ya Fedha na Mipango wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuhitimisha zoezi la kupanda miti katika ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...