TPA KIGOMA 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, Mhandisi Deusidedit Kakoko amesema maboresho makubwa yaliyofanywa katika Bandari ya Kigoma yameanza kuleta matokeo chanya ikiwemo kuongezeka kwa shehena ya mizigo pamoja na mapato. 

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Bandari ya Kigoma, Mhandisi Kakoko alisema shehena na mapato katika bandari hiyo yameongezeka kiasi cha kuipiku Bandari ya Mwanza ambayo ndiyo iliyokuwa ikiongoza kabla ya maboresho hayo. 

Alisema Bandari ya Kigoma ambayo inahusisha bandari zote zilizopo katika Ziwa Tanganyika imeanza kufanyiwa maboresho kuanzia mwaka 2016/17 ikihusisha ujenzi wa magati,  ununuzi wa mitambo,  ujenzi wa maghala na majengo ya abiria pamoja na ujenzi wa ofisi za kisasa za makao makuu ya Bandari hiyo ambazo ziko katika hatua za mwisho kukamilika.

Aliongeza kuwa maborsho hayo yalisukumwa na kasi kubwa ya ongezeko la mahitaji ikilinganishwa na miundombinu iliyokuwepo. 

Alisema bandari za Ziwa Tanganyika zimekuwa kiungo kikubwa cha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani za DRC,  Burundi na Zambia, biashara kubwa ikiwa ni mazao yanayozalishwa Tanzania.

Kutokana na hali hiyo alisema bandari hizo zimekuwa kichocheo kikubwa cha kukuza uchumi wa wananchi wa mikoa inayozunguka Ziwa Tanganyika kwani mazao yao yanapata wanunuzi wengi wanaovutiwa na maboresho ya bandari.

Alisema pia bandari hizo pamoja na kuanza kazi kwa reli kumesaidia kupunguza bei za bidhaa ambazo husababishwa na gharama kubwa za usafirishaji. 

Alisema bado kuna maboresho zaidi yanaendelea katika bandari Kuu ya Kigoma yanahusisha ujenzi wa gati ya maboti ya Kibirizi,  gati ya abiria na makasha na ujenzi wa bandari Kavu ya Katosho.

"Tumekusudia kuifanya bandari ya Kibirizi na Kigoma kuwa ya mizigo ya nje na ile ya Katosho itakuwa ya ndani, " alisema Kakoko. 

Alisema matarijio ya kuongezeka zaidi kwa shehena na abiria ni makubwa kutokana na maboresho ya meli yanayotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Huduma za Meli zikiwemo MV Mwongozo,  MV Liemba na MT Sangara








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...