TPA KIGOMA
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, Mhandisi Deusidedit
Kakoko amesema maboresho makubwa yaliyofanywa katika Bandari ya Kigoma
yameanza kuleta matokeo chanya ikiwemo kuongezeka kwa shehena ya mizigo
pamoja na mapato.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana katika Bandari ya Kigoma, Mhandisi Kakoko
alisema shehena na mapato katika bandari hiyo yameongezeka kiasi cha
kuipiku Bandari ya Mwanza ambayo ndiyo iliyokuwa ikiongoza kabla ya
maboresho hayo.
Alisema
Bandari ya Kigoma ambayo inahusisha bandari zote zilizopo katika Ziwa
Tanganyika imeanza kufanyiwa maboresho kuanzia mwaka 2016/17 ikihusisha
ujenzi wa magati, ununuzi wa mitambo, ujenzi wa maghala na majengo ya
abiria pamoja na ujenzi wa ofisi za kisasa za makao makuu ya Bandari
hiyo ambazo ziko katika hatua za mwisho kukamilika.
Aliongeza kuwa maborsho hayo yalisukumwa na kasi kubwa ya ongezeko la mahitaji ikilinganishwa na miundombinu iliyokuwepo.
Alisema
bandari za Ziwa Tanganyika zimekuwa kiungo kikubwa cha biashara kati ya
Tanzania na nchi jirani za DRC, Burundi na Zambia, biashara kubwa
ikiwa ni mazao yanayozalishwa Tanzania.
Kutokana
na hali hiyo alisema bandari hizo zimekuwa kichocheo kikubwa cha kukuza
uchumi wa wananchi wa mikoa inayozunguka Ziwa Tanganyika kwani mazao
yao yanapata wanunuzi wengi wanaovutiwa na maboresho ya bandari.
Alisema
pia bandari hizo pamoja na kuanza kazi kwa reli kumesaidia kupunguza
bei za bidhaa ambazo husababishwa na gharama kubwa za usafirishaji.
Alisema
bado kuna maboresho zaidi yanaendelea katika bandari Kuu ya Kigoma
yanahusisha ujenzi wa gati ya maboti ya Kibirizi, gati ya abiria na
makasha na ujenzi wa bandari Kavu ya Katosho.
"Tumekusudia kuifanya bandari ya Kibirizi na Kigoma kuwa ya mizigo ya nje na ile ya Katosho itakuwa ya ndani, " alisema Kakoko.
Alisema
matarijio ya kuongezeka zaidi kwa shehena na abiria ni makubwa kutokana
na maboresho ya meli yanayotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Huduma za
Meli zikiwemo MV Mwongozo, MV Liemba na MT Sangara
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...