UONGOZI wa kampuni ya kubashiri matokeo ya Meridian Bet imetoa mkono wa faraja kwenye kituo cha kulea watoto yatima cha Mama wa Huruma kilichopo Madale, Dar es Salaam.

 Afisa Huduma wa jamii wa Meridian Bet, Amani Maeda aliyeambatana na meneja mwendeshaji, Corrie Borman wamesema kampuni yao imeguswa na changamoto ya kituo hicho na kujitoa kukisaidia.

Alisema kwa namna Meridian Bet inavyoguswa na jamii, wameona kusaidia kituo hicho ni wajibu wao kama ambavyo wamekuwa wakifanya kwa jamii yenye uhitaji.

"Tumetoa cement, gypsum poda na pesa kidogo kama kianzio katika ukarabati wa jengo ambalo linatumiwa kama bweni na watoto hawa ambalo tumeelezwa linatumika lakini halijakamilika kujengwa, pia tumetoa vyakula kama sukari, unga, mchele, mafuta na sabuni."

Sister wa kituo hicho, Christina Christopher aliishukuru Meridian Bet na kueleza kwamba wamewapa faraja kipindi hiki ambacho wako kwenye changamoto ya watoto kulala kwenye jengo ambalo halijakamilika.

Alisema baadhi ya watoto wanalazimika kulala katika jengo hilo ili kupunguza msongomano kwenye jengo la awali kwa lengo la kuchukua tahadhari ya janga la corona kwa kupunguza msongamano kwenye jengo la awali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Nimeguswa na hii habari,mungu awazidishie meridian

    ReplyDelete
  2. Mungu awaongezee pale mlipopunguza

    ReplyDelete
  3. Mungu awasaidie meridian bet

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...