Na MWAMVUA MWINYI,PWANI
Mkuu
wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ameuagiza wakala wa maji
vijijini (RUWASA )Mkoa ,kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa miradi
iliyopo kwenye mpango 2019-2021 kwa wakati na kuzingatia ubora na
thamani ya fedha ili jamii inufaike na huduma ya maji.
Aidha
,amezitaka taasisi mbalimbali na wananchi kulipa ankara (bill) kwa
wakati kwani baadhi ya taasisi na wateja wamekuwa wagumu kulipia na
kusababisha miradi mingi kufa.
Alitoa
agizo hilo ,wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya maji mkoa ,uliolenga
kupokea taarifa ya utekelezaji 2019-2021 kutoka RUWASA na kusema
,kufikia Januari 2021 wastani wa wakazi asilimia 73 wanapata maji safi.
"Malengo
hayo ni utekelezaji wa ilani ifikapo 2025 ,hivyo RUWASA kwa
kushirikiana na jamii,viongozi na wadau mkoa kuongeza jitihada ilihali
kufikia malengo ya kumfikia kila mwananchi aweze kupata maji safi."
"Kwa
vijijini wanapata maji kwa asilimia 71 na mijini ni asilimia 84 "
hatujafikia asilimia 11 kwa mijini na 14 vijijini ,ipo miradi
haijakamilika na ipo katika utekelezaji ,RUWASA msimamie miradi hiyo
iweze kuleta tija"alieleza Ndikilo.
Aidha Ndikilo aliitaka jamii kulinda na kutunza miundombinu ya miradi ya maji .
Awali
meneja wa RUWASA Mkoani Pwani ,Beatrice Kasimbazi alieleza ,mkoa
umepanga kutekeleza miradi 65 kwa gharama ya sh .bilioni 18.782.137.8
kwa kipindi cha mwaka 2021-2022 ambapo miradi mipya ni 17,upanuzi miradi
14 na ya ukarabati ni 34.
Kasimbazi
alieleza kwamba,miradi inayoendelea kuanzia Julai 2019-februari 2021 ni
miradi 48 ambayo inagharimu bilioni 9.829.086 na itanufaisha wakazi
99,334.
"Miradi mipy 16
gharama bilioni 8.403.232.5 na itanufaisha wakazi 77,760 pamoja na
miradi 32 bilioni 1.425.853 kunufaisha wakazi 21,574.
Nae
mkuu wa Wilaya ya Rufiji Luteni Kanal Patrick Sawala alieleza,
malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi wake Wilaya hiyo ni bili kubwa
za maji kuliko uhalisia wa matumizi.
Kwa
upande wa mwenyekiti wa halmashauri ya Mafia ,Juma Salum alisema
wananchi wa Mafia wanalalamikia bili kubwa katika vituo vya maji
,wanaiomba mamlaka husika isimamie hilo .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...