*SALAAM ZA WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA
JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO MHE. DKT. DOROTHY.O GWAJIMA KUELEKEA SIKU
YA WANAWAKE DUNIANI TAREHE 08/03/2021 INAYOFANYIKA KIMKOA NCHINI
TANZANIA.*
Napenda
kuwapongeza na kuwatia moyo wanawake wote nchini Tanzania kwa nafasi yao
kama wanawake kwenye kuchangia maendeleo ya taifa hili ngazi zote.
Nawapongeza kwa Kauli Mbiu nzuri ya siku hii ya “Wanawake katika
Uongozi; Chachu Kufikia Dunia yenye Usawa.
Nawahakikishia
kuwa Serikali ya Tanzania inajali wanawake na iko mstari wa mbele
kutekeleza mipango endelevu ya maendeleo yenye nguzo za kisheria na
kisera. Kwa mfano;
1. Serikali
inatekeleza mpango wa kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia mikopo
ambapo kwa mwaka 2019/2020 imetoa mikopo ya thamani ya Tsh Bilioni 23.8
iliyonufaisha Vikundi 6859 vya Wanawake Wajasiriamali.
2. Serikali
inatekeleza mpango wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa watoto na
wanawake (MTAKUWWA) ambapo kuna Kamati rasmi hadi ngazi ya Jamii, Wilaya
na Mkoa. Kamati hizi zinasimamia, zinaelimisha na kufuatilia vitendo
vyote vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na kuchukua hatua stahiki.
3. Kwa upande wa elimu Serikali inajali watoto na sasa inatekeleza sera ya elimu bila malipo kwa watoto wote wa Kitanzania.
4. Serikali
haijawaacha nyuma wanawake kwenye nafasi za uongozi ngazi zote kuanzia
Mheshimiwa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu, Mheshimiwa Naibu Spika wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Akson, Waheshimiwa
Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi na wengine wengi.
5. Kwenye huduma za Afya bajeti karibu 75% inazingatia huduma za afya kwa wanawake wajawazito na watoto.
Hivyo,
kwa mifano hii michache napenda kuwahakikisha Wanawake na Watoto kuwa
wako salama chini ya Uongozi wa Rais Dkt John Pombe Magufuli ambaye
Serikali yake siku zote imeendelea kuzingatia mustakabali wa maendeleo
na ustawi wao.
Kwa salaam
hizi fupi naomba niwatakie Wanawake wote Sikukuu njema yenye furaha,
amani na upendo huku wakikumbuka kuwa „Wanawake katika Uongozi; Chachu
Kufikia Dunia yenye Usawa”. Aidha, Wito wangu kwa Wanawake wote ambao
tupo kwenye nafasi mbalimbali za uongozi tuzidi kushikamana na
kushirikiana kuzingatia kusimamia haki, usawa na maslahi ya wanawake na
watoto daima.
Mungu Ibariki Siku ya Wanawake Duniani Tarehe 08/03/2021.
*Dkt. Dorothy Gwajima (Mb)* *WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO*
*07/03/2021*
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...