Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa fursa na kuwaamini zaidi wanawake na watoto wa kike katika nafasi za uongozi, siasa, masomo na katika taasisi za umma kwa kuwa siku zote wameonesha upendo, uchapakazi, uzalendo, umakini na utekelezaji uliotukuka.
 
 Ikumbukwe Serikali imetekeleza kivitendo na itaendelea kufanya hivyo kwani leo wanawake wameendelea kuvunja rekodi ya kushika nafasi kubwa za kiuongozi hapa nchini akiwemo Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhandisi Zena Ahmed Said ambaye kwa sasa ni mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar. Tunawapenda sana wanawake na hakika mnaweza.

Kwa kuwa leo ni Machi 8, Siku ya Wanawake Duniani, kwa niaba ya Serikali tunawatakia wanawake wote wa Tanzania heri ya siku hii na waendelee kufanya  tafakuri juu ya mchango wao zaidi kwa Taifa na dunia. Tunawapenda sana

Dkt. Hassan Abbasi
Msemaji Mkuu wa Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...