VIONGOZI wa kidini na wale wa vyama vya siasa Zanzibar wamesema kuwa malim Seif sharif Hamad ni mtu aliyemaliza muda wake wa kuishi katika ulimwengu akiwa amewacha mafanikio  makubwa.

Hayo wameyasema katika kanisa la PEFA church of Zanzibar nje kidogo ya mji wa Zanzibar  huko Kisauni wakati wakitoa historia ya marehemu maalim Seif Sharif Hamad  katika hafla ya kumbukumbu ya kusherekea maisha ya kiongozi huyo aliyekuwa  Mwenyekiti wa Chama cha ACT wazalendo.

Viongozi hao wamelezea kuwa wanakila aina ya sababu ya kumkumbuka na kumuenzi kiongozi huyo kutokana na kile walichokisema wema mkubwa aliowatendea wazanzibar.

“Maalim alikuwa kiongozi wa aina ya kipekee na mwenye kuipenda Zanzibar na watu kutoka ndani ya moyo wake kwa nini tusimkumbuke.” walisema viongozi hao.

Naibu Katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Zanzibar  Katherin Pitanao   alisema kuwa kiongozi huyo  amemaliza muda wake   akiwa na kila alama ya wema.

Alisema  Malim seif amekwenda kwa baba akiwa ameiacha Zanzibar salama na wala hawana  mashaka na  mtu aliyetangazwa kushika nafasi ya malim Seif wana imani Zanzibar itatengamaa. 

Katherina ameleza ana imani kuona Zanzibar inakwenda mbele zaidi na hana mashaka na Dk husein Mwinyi kwani ameonesha wazi kutaka umoja , maendeleo na kuinua uchumi imara wa Zanzibar.

Alisema hana mashaka na viongozi waliopo sasa anajua wanayo dhamira ya kweli ya kuitumika nchi hii sambamba na kuendelea  kuwa na mshikamano wa pamoja. 

 “Sisi tuliamini maalim Seif ameacha mali kwa muda aliotumikia nchi hii  tuliamini ameacha  majumba Dubai ana majumba Dar es Salaam ana majumba Zanzibar lakini hapana amekwenda akiwa maskini amekwenda kama alivyokuja hakuacha mali yeyote”Alisema Katherina .

Muwakilishi kutoka katika dini ya kikristo Joshua Goma amesema malim amekuwa mfano mzuri kwa kuwaunganisha na kuwaeka pamoja  watu ambao walikuwa wametofautiana kutokana na vyama vyao .

Amesema ni wajibu wa vyama vya siasa kuchukua nafasi ya kunganisha watu bila ya kujali itikadi zao za kisiasa kwani kufanya hivyo ni kuwa na uono wa mbali . 

Naibu Katibu mkuu wa Chama Cha ACT Wazalendo  Nassor Ahmed Mazrui amesema Marehemu maalim Seif Sharif  Hamad ameacha urathi ambao unataka  kuendelezwa ili Zanzibar ifike pale inapotaka kwenye uchumi wa bluu.

Mazrui amesema bila ya kuendelezwa yale aliyoyacha umoja maelewano na mshikamano  Zanzibar haiwezi kufika pale inapotakiwa kufika.

Kwa upande wake afisa  kutoka ofisi ya Makamo wa kwanza wa rais Makame Khatib Makame amezitaka tasisi zote nchini kuiga wigo wa kumkumbuka Maalim Seif kwa kwa kuyaenzi yale mazuri aliyoyawacha.

“Tumkumbuke Maalim Seif kwa azma yake ya kuleta umoja na mshikamano nchini Sote tusimame kwa msingi wa kuepuka rushwa na ubadhirifu na kuweka upendo miongoni mwetu.”alisema Makame.

Amesema kuwepo kwake kumeleta mashirikiano ya msingi wa kuwaleta watu pamoja na Zanzibar imepata mafanikio ya kutosha.

 “Tunamkumbuka Maalim Seif kwa kutuachia ushirikiano hatuna budi kila mmoja kuendeleza kwa nguvu zote”alisema Makame.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...