Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv


Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani 2021 yenye kauli mbiu ya usawa kwa wote, Shirika la Posta Nchini limesema wanawake ni chachu ya maendeleo na ongezeko la pato ndani ya taasisi hiyo.

Aidha, Shirika la Posta limesema  litaendelea kutoa kipaumbele kwenye nafasi kubwa ya uongozi kwa wanawake katika taasisi hiyo pale inapohitajika.

Maadhimisho ya siku wanawake duniani yanafanyika kila ifikapo Machi 08, ya kila mwaka na kwa mwaka huu yaliweza kuambatana na maandamano yenye mabango mbalimbali yenye jumbe za kuhamaisha ushirikishwaji wa wanawake kwenye sekta muhimu nchini yakihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu.

Akizungumzia siku ya wanawake duniani, Afisa Mwandamizi wa Shirika la Posta Aneth Mdimu amesema Shirika la Posta litaendelea kuwa na usawa kwa wote katika kutoa ajira kwa wanawake.

Amesema, katika taasisi yao usawa kwa wote imekuwa ni sera yao kubwa sana na wamekuwa na wanawake wengi sana katika vitengo mbalimbali wakifanya kazi zao kwa ustadi mkuu.

" Ukiangalia katika taasisi yetu kuna Mkurugenzi wa Kibiashara ambaye ni mwanamke  bodi ya wakurugenzi iliona kuna haja ya kuwa mwanamke kwani wanaweza kwa hilo tunawashukuru sana,"

Mdimu amesema, ukiangalia katika ngazi ya mikoa kuna wanawake wengi wanaosimamia taasisi yao  hilo limetokana na Uongozi wa Shirika la Posta kuona wanawake wanatosha katika kuliendesha gurudumu la maendeleo.

" Asilimia kubwa ya pato la taasisi tunaingiza sisi wanawake, tupo katika kila kitengo na ukimkuta mwanamke akifanya kazi zake bila wasiwasi wala kuhitaji msaada kutoka kwa mtu yoyote, tunajivunia," amesema

Aidha,amesema kuwa wanawake katika shirika la Posta wamejizatiti kufanya kazi kwa uweledi mkubwa bila kuwezeshwa, wamejipanga kuhakikisha wanafikisha asilimia 98 ya wanawake katika taasisi hiyo.

Mdimu ameongezea, wanaishukuru taasisi kwa kuwajali na kuwalinda wanawake hata kipindi cha afya ya uzazi imekuwa inamtunza Mwanamama kwa kupata stahiki zake zote na hata akirejea kazini amekuwa anapata muda wa kunyonyesha.

Machi 08, kila mwaka dunia nzima imekuw inaadhimisha siku ya wanawake dunian wakija na kauli mbiu mbalimbali zikihamasisha wanawake wapatiwe usawa katika sekta mbalimbali ambapo kwa mwaka huu imejikita katika "wanawake na uongozi chachu ya kufikia dunia yenye usawa"



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...