.Baadhi ya watumishi wanawake wa MNH-Mloganzila wakifanya usafi katika mazingira ya nje ya hospitali ikiwa ni kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 8.
Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila Dkt. Julieth Magandi (kushoto) akiongoza zoezi la usafi wa mazingira lililofanyika leo hospitalini hapa.





Wafanyakazi wanawake wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila wamefanya usafi wa mazingira ya nje ya hospitali ikiwa sehemu ya shughuli za kijamii na kujitolea katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili–Mloganzila Dkt. Julieth Magandi amesema lengo ni kuimarisha usafi wa mazingira hasa katika maeneo yote yanayozunguka hospitali .

“Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) kwa kushirikiana na uongozi wa hospitali tumeshirikiana kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya hospitali yetu ili wateja wetu wanaofika kupata huduma wawe katika mazingira safi na salama” amesema Dkt. Magandi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake TUGHE Tawi la Mloganzila Bi. Sperancia Mhapa ameishukuru uongozi wa hospitali pamoja na wanawake wote waliojitokeza na kufanikisha zoezi la kufanya usafi na kuahidi kuwa watahakikisha shughuli za kijamii zinakua endelevu.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani mwaka huu ni “Wanawake katika uongozi ni chachu kufikia Dunia yenye usawa”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...