Na Amiri Kilagalila, Njombe.

Watu wanne akiwemo mkuu wa chuo cha uuguzi Lugarawa Steven Mtega (39) wamefariki dunia kwa kuzama kwenye mto Lupali wakiwa kwenye gari waliyokua wakisafiria kata lugarawa wilayani Ludewa mkoani Njombe.

Akizungumza kwa njia ya simu jana mganga mkuu  wa wilaya ya Ludewa dkt Stanley Mlay,alisema tukio hilo limetokea febuari 27 majira ya usiku marehemu hao walikua kwenye gari aina ya harrier ambapo walikua Lugarawa kwenye mambo yao ya mapumziko.

"Walipata ajali kwenye mto lupali huu mto sasa hivi una maji mengi kwa sababu ya mvua zinavyonyesha walikua watu wanne kwenye mambo yao ya mapumziko Lugarawa na dereva alikua huyo mkuu wa chuo wakasema wabadilishe maeneo waende Mundindi sasa walivyofika maeneo hayo ndo wanaingia mtoni" alisema Mlay.

Mlay aliwataja marehemu wengine kuwa Marko Mpete,fundi umeme wa Lugarawa
Merk Mwalongo(35)mjasiriamali
Rukia Mfaume(28) alikuwa mhasibu wa mradi wa umeme wa Akra Lugarawa

Hata hivyo alisema miili ya marehemu hao iko chumba cha kuhifadhia maiti(Mochwari)Hospital ya Lugarawa ikisubiri taratibu za mazishi kukamilishwa.

Naye diwani wa kata ya Lugarawa Erasto Mhagama,akizungumza kutokea kwa tukio hilo alisema tukio hilo limetokea mpakani kwa kijiji cha shaurimoyo na kijiji cha amani.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...