Mkuu wa
Wilaya ya Arusha Mheshimiwa Kenani Kihongosi amefanya ziara ya kikazi
Kukagua meadi wa Maji wa Bilioni 520 akiambatana na Madiwani wa jiji la
Arusha wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Jijibla Arusha Mheshimiwa
Maximillian Iraghe pamoja na watendaji wa kata katika Jiji la Arusha.
Mheshimiwa
mkuu wa Wilaya Amewaeleza Madiwani pamoja na watendaji kata kwenda na
Kuwafafanulia wananchi Hatua nzuri ya Mradi ilipofikia na wawaeleze
wananchi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais
Dr. JOHN POMBE MAGUFULI Ipo Kazini kuhakikisha maendeleo makubwa
yanawanaufaisha wananchi.
Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amewapongeza
Mamlaka ya Maji AUWSA na Kuwaagiza wakamilishe mradi kwa wakati ili
Wananchi wafurahie Matunda ya Serikali yao.
Mkuu wa Wilaya pamoja
na Madiwani na watendaji wa kata wamemshukuru Mheshimiwa Rais DR JOHN
POMBE MAGUFULI kwa kutoa fedha nyingi katika mradi huo na wamemuombea
kwa Mwenyezi Mungu azidi KUMPA Nguvu na Afya Katika kuwatumikia
WATANZANIA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...