Serikali imetenga shilingi  milioni 311.9 zitakazotumika  kuchonga Barabara yenye urefu wa kilometa 20 katika hifadhi ya Taifa  Rumanyika karagwe na kilometa 51 katika  Hifadhi ya Taifa ya Ibanda Kyerwa katika mwaka wa fedha 2020/2021.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja wakati akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Kyerwa Mhe. Innocent Sebba  Bilakwate (CCM)  ambaye alihoji kuhusu mpango wa  Serikali  wa kuweka miundombinu mizuri ya Barabara katika hifadhi hizo Ili kuvutia watalii.

Akijibu Swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Damas Ndumbaro  ,Mhe. Masanja ameeleza kuwa hifadhi za Taifa za Ibanda Kyerwa na Rumanyika karagwe  zilianzishwa kupitia tangazo la Serikali Na 509 na 510 la tarehe 5/7/2019 .

Amesema hifadhi hizo zilitokana na kupandishwa hadhi kwa yaliyokuwa mapori ya akiba ya Ibanda na Rumanyika .

"Ili  kuwezesha hifadhi hifadhi hizo kufikika kwa urahisi Serikali kupitia  TANROADS na TARURA iliyokuwa ikitengeneza Barabara mbalimbali zinazorahisha kufika kwa watalii katika hifadhi hizo , Barabara hizo ni pamoja Mgamkorongo iliyopo wilaya ya korogwe hadi murongo wilayani Kyerwa yenye urefu wa kilometa 112 ambayo inafanyiwa   matengenezo na TANROADS kila mwaka na imewekwa  katika mpango wa Kujengwa kwa kiwango cha lami katika mwaka wa fedha 2020/2021" Amesisitiza Mhe.Mary Masanja.

Aidha, amesema jitihada hizo za kuboresha miundombinu ya Barabara katika hifadhi ya Taifa Ibanda Kyerwa na Rumanyika Karagwe na maeneo mengine yote ya hifadhi zitasaidia kuweka Mazingira mazuri  yatakayowezesha hifadhi hizo kutembelewa na watalii wengi wa maeneo ya karibu pamoja na wageni kutoka nchi jirani.

Kuhusu ulinzi wa maeneo hayo  ameeleza  kuwa wizara imekuwa ikiyaanisha maeneo yote na kuweka mipaka.

" Katika hifadhi ya Ibanda Kyerwa na Rumanyika tulifanya tathmini baada ya  wataalamu wetu kuainisha mipaka, utekelezaji wake tunaendelea nao kwa kuandaa Mazingira ya kuwapeleka wataalamu kwa ajili ya gharama za uthamini na kuanisha maeneo ambayo yanachangamoto za uhifadhi " Amesisitiza.

 


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Francis Masanja akiwasili katika viwanja vya Bunge kuhudhuria mkutano wa 3 wa Kikao cha 5 cha Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapema leo April 08, 2021 Jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...