Ndugu Wananchi, Awali ya yote nachukua fursa hii kuwatakia watumiaji wote wa huduma za afya nchini Tanzania Heri ya Siku ya kumbukizi ya Hayati Abeid Amani Karume leo tarehe 7/04/2021. Tumkumbuke kwa ushujaa na uzalendo wake daima.

Aidha, napenda kutoa Shukrani kwa Wananchi wote ambao wamekuwa wakiwasilisha Pongezi, Maoni na Kero zao kupitia mifumo mbalimbali ya mawasiliano ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ikiwemo kwa barua, mitandao yetu ya kijamii, simu na ujumbe mfupi kupitia namba 199. Nikiri kuwa taarifa hizo zimeendelea kutoa mchango mkubwa katika kutambua maeneo yanayofanya vizuri na yale yenye changamoto.

Ndugu Wananchi, Vilevile, nawashukuru maelfu ya Wananchi ambao pale wanapoona hawakupata msaada kwenye ngazi ya Kituo, Halmashauri, Mkoa au Wizara kupitia namba husika zilizotangazwa wamekuwa wakizingatia kunitumia ujumbe mfupi kwenye simu yangu mimi Waziri ya 0734124191 kama nilivyoitangaza Disemba 19, 2020.

Ndugu Wananchi, Napenda kuwakumbusha kuwa, kwa pongezi na kero za huduma za afya kamwe msikose mahali pa kusemea bali muendelee kutumia mifumo ya mawasiliano ya haraka huku mkizingatia maelekezo yaliyotolewa. Mahsusi kwa simu yangu Waziri wa Afya ya 0734124191 mawasiliano haya ni kwa ujumbe mfupi tu.

Nawahakikishia kuendelea kujibu na nikiona inafaa nitapiga simu au kutoa maelekezo kwa wasaidizi wangu wafuatilie na kusimamia jambo hilo na kunipa mrejesho.

Kwenu watumishi wataalamu wa afya, Natoa pongezi kwa wale wote ambao wamekuwa wakijituma kwa bidii kuwahudumia wateja wanaohitaji huduma za afya. Hakika kupitia maoni ya wateja tumeendelea kuwatambua watumishi wengi wenye moyo wa uzalendo na upendo katika kutimiza wajibu wao. Wale wenye changamoto nao tumeendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa mujibu wa Sheria, Taratibu na Kanuni.

Ndugu Wananchi, Natoa Shukrani za dhati kwa ushirikiano wenu na tuendelee kushirikiana daima.

Dkt. Dorothy Gwajima.
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO.
07/04/2021.
Simu. 0734124191 (tuma ujumbe mfupi tu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...